Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 5 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 83 2023-02-06

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE.ANTON A. MWANTONA aliuliza:-

Je, ni lini mradi wa REA II utamalizika kwa Vijiji 25 vilivyobakia katika Jimbo la Rungwe?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Anton Albert Mwantona, Mbunge wa Rungwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji 25 vilivyobaki katika Jimbo la Rungwe vitapatiwa umeme kupita Mradi wa REA III mzunguko wa pili ambapo kwa sasa Mkandarasi yupo eneo la mradi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa mkataba, Mkandarasi wa kazi hiyo (ETDCO) atakamilisha kazi kwenye vijiji hivyo Mwezi Desemba, 2023. Ahsante sana.