Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Latifa Khamis Juwakali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI aliuliza: - Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya masomo ya dini kutokuwa principal pass ya kujiunga na Stashahada na Shahada?

Supplementary Question 1

MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa, sasa Serikali imetuelezea kwamba kuna vyuo mbalimbali ambavyo vinatoa elimu ya juu ambayo inazingatia hiyo principal pass. Je, hamuoni sasa Serikali kuandaa Mpango maalum kupitia TCU ambao ndiyo wadhibiti ubora wetu wa Elimu ili waweze kuwashauri sasa Vyuo Vikuu vyetu waweze kuliingiza ili somo la dini liwe kama ni miongoni mwa Principal pass?

Swali langu la pili, kwa kuwa masomo haya ya dini yanawajenga vijana wetu kimaadili lakini pia yanawajenga wanafunzi wetu wetu kimaadili lakini na kiimani. Je, hatuoni sasa kulitoa hili somo la dini kwamba siyo miongoni mwa principal pass ambazo zitamsaidia mwanafunzi kujiunga na Chuo Kikuu, hatuoni sasa tunawaandaa wanafunzi wengi ambao wakimaliza Vyuo Vikuu watakuwa hawana maadili mazuri kwa sababu wanafunzi hawatalisoma hili kama ni somo la msingi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Latifa Juwakali kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyokwisha kueleza kwenye majibu ya msingi kwamba masomo haya ya dini yanatumika kwenye baadhi ya Vyuo na kwenye baadhi ya program. Hatuwezi program zote tukasema kwamba ziingize masomo ya dini, kwa sababu itategemea na program gani mwanafunzi anayokwenda kusoma. Kwa hiyo, tumebeba ushauri huo alioutoa lakini ninaomba nimpe taarifa Mheshimiwa Mbunge kwamba TCU jukumu lake ni kudhibiti, kufanya Ithibati ya ubora wa masomo yanayotolewa na siyo kupanga kwamba program gani iingizwe na kwa requirement zipi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimezungumza zile Senate ndizo zenye wajibu wa kupanga namna gani requirements zinazotakiwa kwenye program husika. Kwa hiyo, tunalibeba suala hili la kuona namna gani masomo yetu ya dini yanaweza yakaingizwa kwenye baadhi ya hizo program kwa kadri tutakavyoona inafaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti nakushukuru sana.