Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 5 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 82 2023-02-06

Name

Latifa Khamis Juwakali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI aliuliza: -

Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya masomo ya dini kutokuwa principal pass ya kujiunga na Stashahada na Shahada?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia napenda kujibu swali la Mheshimiwa Latifa Khamis Juwakali Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa utaratibu wa uendeshaji wa elimu ya Chuo Kikuu hapa nchini na katika nchi nyingine duniani, Mabaraza ya Vyuo Vikuu (Seneti) yamepewa mamlaka ya kisheria kuweka vigezo mahsusi vya udahili kwa kila programu ya masomo kwa ngazi husika (Specific Program Requirements).

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hapa nchini, principal passes za masomo ya dini zinatambuliwa kama vigezo mahsusi vya kujiunga na baadhi ya program za masomo kwa ngazi ya Stashahada na Shahada ya kwanza. Mfano, baadhi ya Vyuo Vikuu ambavyo vimekuwa vikitumia masomo ya dini kama kigezo kimojawapo cha kujiunga na program za masomo ni pamoja na Chuo Kikuu cha Kiislam cha Morogoro; Chuo Kikuu cha Zanzibar; Chuo Kikuu cha Arusha; Chuo Kikuu cha Mt. Yohana cha Tanzania; Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi; Chuo Kikuu Huria cha Tanzania; Chuo Kikuu Kishiriki cha Tumaini Dar es Salaam na Chuo Kikuu cha Iringa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.