Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bahati Keneth Ndingo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. BAHATI K. NDINGO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwajengea uwezo Wahitimu wa Vyuo nchini ili waweze kushindana katika soko la ajira?

Supplementary Question 1

MHE. BAHATI K. NDINGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa, wameshaanza mapitio ya mitaala, ni kwa namna gani wameweza kushirikisha sekta binafsi katika mapitio ya mitaala hiyo ikiwa wao ndio waajiri wakubwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, tunatambua kwamba elimu ya ufundi kwa sasa ni muhimu ili kuwawezesha wahitimu kujiajiri na kuajiriwa. Sasa Serikali ina mkakati gani kuhakikisha wanaanza kutoa mikopo kwenye vyuo vyetu vya ufundi nchini? Ahsante. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Bahati Keneth, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyoeleza katika majibu ya msingi, kwamba kupitia mradi huu wa HEET ambao ni wa zaidi ya Dola milioni 425, tunafanya maboresho makubwa na mapinduzi makubwa katika sekta ya elimu. Miongoni mwa mapinduzi hayo ni katika kuboresha mitaala yetu iliyopo sasa. Katika uboreshaji wa mitaala hii, ushirikishaji wa wadau, kama nilivyozungumza kwenye jibu la msingi, ni wa kiasi kikubwa ikiwemo na sekta binafsi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge pamoja na Bunge lako Tukufu, ushirikishwaji wa wadau mbalimbali wakiwemo sekta binafsi tunauzingatia kwa kiasi kikubwa na ndiyo maana tunafanya kitu kinaitwa tracer study and needs assessment. Lengo kuu ni kuhakikisha kwamba tunapata mahitaji, lakini vilevile tunawashirikisha wadau.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo la pili, nazungumzia suala la mikopo katika kada ya kati. Hili suala tayari tulishalizungumza hapa Bungeni na tulisema wenzetu wa NMB tayari wameshaingia kwenye utaratibu huu. Wametenga zaidi ya Shilingi bilioni 200 katika mwaka huu wa fedha 2022/2023, lakini sisi kama Serikali katika mwaka 2023/2024 tunakusudia sasa kutenga fungu kwa ajili ya mikopo katika kada hii ya kati, nakushukuru sana. (Makofi)