Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 5 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 81 2023-02-06

Name

Bahati Keneth Ndingo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. BAHATI K. NDINGO aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwajengea uwezo Wahitimu wa Vyuo nchini ili waweze kushindana katika soko la ajira?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bahati Keneth Ndingo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi ujulikanao kama, Higher Education for Economic Transformation (HEET), inaendelea na maandalizi ya uboreshaji wa mitaala iliyopo na uandaaji wa mitaala mipya zaidi ya 290 katika programu za kipaumbele cha Taifa ili kuwajengea uwezo wahitimu kuhimili ushidani wa soko la ajira ndani na nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua inayoendelea ni ukusanyaji wa maoni (tracer study and needs assessment) kutoka kwa wadau mbalimbali wa elimu ili kubaini mahitaji halisi. Mitaala hiyo iliyoboreshwa inatarajiwa kuanza kutumika katika mwaka wa masomo 2023/2024, nakushukuru.