Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FATMA H. TOUFIQ aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kuzuia matukio ya mauaji, kujiua na ukatili uliokithiri hasa kwa wanawake na watoto?

Supplementary Question 1

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali ya nyongeza. Niishukuru sana Serikali kwa majibu mazuri, nina maswali mawili ya nyongeza: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwa na program maalum hasa kwa kutumia mapolisi kata ili waweze kutoa elimu kwa jamii kuweza kupunguza masuala ya ukatili?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili. Kwa kuwa kuna baadhi ya wananchi wamekuwa wakisambaza picha ambazo zinaonesha matukio mbalimbali ya ukatili katika mitandao ya kijamii na picha nyingine zimekuwa zikikiuka haki za binadamu na kutweza utu wa wale ambao ni wahanga wa ukatili: Je, Serikali haioni upo umuhimu wa kuwa na namba maalum ya Serikali ambayo matukio yale yatapelekwa kule badala ya watu wachache kusambaza picha hizi katika mitandao?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Fatma Toufiq, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua umuhimu wa kuendelea kuimarisha elimu kwa ajili ya jamii nzima kupitia Polisi wetu wa Kata. Kwa kutambua hilo, ndiyo maana kuanzia mwaka 2022 Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan imeridhia kutoa ajira zaidi ya Askari Wakaguzi Sasaidizi 3,200 na kupangiwa kwenye kata. Tumeanza kuona baadhi ya kata wameanza kufanya vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaomba Waheshimiwa Wabunge na viongozi wetu kwenye Wilaya na Halmashauri kuwatumia Polisi Kata hawa, hasa wanapokuwa na vikao vyao, mikutano ya hadhara ili waendelee kutoa elimu. Hii itasaidia kupunguza uhalifu kwenye maeneo mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, juu ya ushauri alioutoa wa udhibiti wa usambazaji wa picha zinazokiuka haki na maadili, tunapokea ushauri huo ili tuweze kuufanyia kazi. Ni kweli, baadhi ya picha zinazooneshwa kwenye mitandao ya kijamii nyingine ziko vibaya sana, badala ya kusaidia zinaharibu kabisa. Kwa hiyo, tunaupokea ushauri huo ili tuweze kuufanyia kazi, ahsante sana.

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FATMA H. TOUFIQ aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kuzuia matukio ya mauaji, kujiua na ukatili uliokithiri hasa kwa wanawake na watoto?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hili wimbi kubwa la ukatili na tabia zote mbaya katika jamii: Je, Serikali haioni sasa iko haja ya kuimarisha Polisi Jamii kwenye vijiji ili angalau huo ukatili uweze kutambulika kwa haraka zaidi? Ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Thea Ntara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwamba swali hili linakaribiana sana na swali lililoulizwa na muuliza swali la msingi. Ni kweli, sasa hivi tumeweka hawa Wakaguzi wa Polisi kama viongozi kwenye ngazi hizo za kijamii, lakini pia wapo Polisi wa kawaida wenye vyeo vya chini ili kushirikiana na hawa Polisi Kata. Kwa hiyo, ushauri alioutoa Mheshimiwa tunauzingatia na ndiyo maana tutaendelea kuimarisha eneo la Polisi Kata kweye kata zetu zote ili waweze kutimiza wajibu wao huu wa msingi, ahsante sana.