Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 79 2023-02-06

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FATMA H. TOUFIQ aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kuzuia matukio ya mauaji, kujiua na ukatili uliokithiri hasa kwa wanawake na watoto?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Fatma Hassan Toufiq, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Jeshi la Polisi itaendelea kuwakamata watu wote wanaotenda makosa yakiwemo ya mauaji na ukatili na kuwafikisha Mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake. Uchunguzi wa Jeshi la Polisi unaonesha kuwa matukio haya kwa kiasi kikubwa yanasababishwa na watu kujichukulia sheria mkononi, imani za ushirikina, wivu wa mapenzi, migogoro ya ardhi, migogoro kwenye ndoa, kugombania mirathi, ulevi na mmomonyoko wa maadili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Jeshi la Polisi itaendelea kutekeleza mkakati wa kutoa elimu na mafunzo kwa jamii ili wananchi wafuate sheria za nchi katika kutatua migogoro inayojitokeza au wanapodai haki zao. Aidha, wananchi wanaombwa kuwashirikisha viongozi wa kijamii, kimila, kisiasa na kiserikali, wazee au watu maarufu wanaotambulika na kuheshimika ili kuwaasa ipasavyo na hivyo kuepuka kuvunja sheria za nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.