Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza:- Je, ni kwa kiwango gani task forces zimepunguza tatizo la uvuvi haramu katika Ziwa Victoria kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa majibu ya Serikali. Kutokana na Takwimu za Serikali yenyewe, hali ya Ziwa Victoria hususani upatikanaji wa mazao ya samaki ni mbaya sana. Kulingana na viwango ambavyo tumejiwekea katika Ziwa lolote samaki wazazi wanapaswa kuwa kati ya asilimia 3-5 lakini kwa Takwimu ambazo zimetolewa na Serikali hii katika Ziwa Victoria samaki wazazi wako chini ya asilimia 0.85. Swali la kwanza; sasa naomba Serikali inipe majibu upungufu huo hausiani na uvuvi haramu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Task Force zimekuwa zikiendelea Ziwa Victoria, hawa ambao wanatumwa kwenda kufanya hiyo kazi ni wasomi, lakini hawana weledi wowote na masuala ya uvuvi. Matokeo yake wamekuwa wakikamata hizo zana haramu wanawapiga faini zisizo na Kanuni wala Sheria wala sijui nini, baada ya kuwapiga faini wanawarudishia zile zana haramu ambazo zinasadikiwa kuwa ni zana haramu.

Je, Serikali haioni kwamba inaendekeza huo uvuvi wa haramu kwa kutumia pesa ya walipakodi wa Tanzania? (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Oscar Ishengoma Kikoyo, Mbunge wa Muleba Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, upungufu hauhusiani na uvuvi haramu? Kwa namna yeyote ile upungufu wa samaki wazazi unahusiana na uvuvi haramu na ndiyo maana tumeweka mkakati shirikishi kama Serikali kupitia Vyombo vyetu vyote na sasa tunakwenda katika kutekeleza mkakati ule ambao utakwenda kunusuru na kulinda moja; samaki wazazi lakini mbili rasilimali nzima na kwa hivyo itapelekea kupatikana kwa uendelevu wa rasilimali hii muhimu kwa Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, amehusianisha juu ya vitendo vya baadhi ya maafisa wetu wasiokuwa waaminifu na waadilifu. Nakiri yawezekana wako maafisa wanaofanya vitendo vya kinyume na maelekezo na maagizo ya Serikali. Tuko tayari kushirikiana na Mheshimiwa Mbunge, ikiwa anafahamu watumishi wanaofanya hivyo, Taratibu, Sheria na Kanuni za Kiutumishi zipo, nataka nimuahidi yeye kwamba tutachukua hatua madhubuti kwa yeyote ambaye anashiriki katika kuharibu operations na shughuli za Kiserikali zenye lengo jema kabisa la kulinda rasilimali za nchi hii, ahsante sana. (Makofi)

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza:- Je, ni kwa kiwango gani task forces zimepunguza tatizo la uvuvi haramu katika Ziwa Victoria kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kwa kuwa Serikali ina mpango wa kutoa mikopo ya zana za kisasa za uvuvi kama boti pamoja na pesa kwa ajili ya kufanya uvuvi wa kuvua samaki kwa njia ya vizimba kama njia ya kuzuia uvuvi haramu. Je, ni lini sasa mikopo hii itawafikia wavuvi wetu? Nashukuru sana. (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Joeseph Mkundi, Mbunge wa Ukerewe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imejidhatiti katika kuondoa uduni na kero ya Wavuvi kutumia vyombo hafifu na kwa hivyo kupelekea kupatikana kwa vyombo vya kisasa sasa ni lini tunawapitia?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari hatua za kimanunuzi zimekalika. Tunazo boti takribani 160 za kisasa zitakazogawiwa kwa wanufaika Wavuvi waliotimiza viwango ambavyo viliwekwa na Serikali na miongoni mwa Wavuvi hao wapo wa kule Ukerewe. Boti hizo zitakuwa ni za kisasa zenye fish finder, kwa maana kifaa maalumu kinachoelekeza wapi samaki alipo lakini pia vilevile kitakuwa nae neo la kuhifadhia samaki lisilopungua tani moja, kitakuwa na GPS na vifaa vingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mbili, Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan imetoa pesa takribani bilioni 20 kwa ajili ya zoezi la ufugaji wa samaki kuongeza uzalishaji wa samaki aina ya sato. Walengwa ni pamoja na vikundi vya vijana na akinamama.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza:- Je, ni kwa kiwango gani task forces zimepunguza tatizo la uvuvi haramu katika Ziwa Victoria kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita?

Supplementary Question 3

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante sana kwa kuniona. Wizara katika siku za karibuni ilitoa nafasi kwa Vikundi Mbalimbali vya Uvuvi viweze kuomba mikopo katika Wizara hiyo. Swali langu, je, ni lini fedha hizo zitatoka ili ziweze kuwanufaisha wananchi wetu wakiwemo wananchi wa Wilaya ya Kilwa?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ndulane, Mbunge wa Kilwa Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, miongoni mwa wanufaika wa mikopo ile ya Serikali ya Awamu ya Sita kwa Wavuvi inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan ni Wavuvi wa Kilwa, watapata boti hizo na tayari taratibu zimekwishakamilika, orodha ya wanufaika iko tayari tuta- share na Waheshimiwa Wabunge wote ili muweze kuona kile mlichokiomba ni hiki kimepatikana na kwa kusudi hilo muweze kuwafikishia walengwa wajipange ili tuweze kutekeleza kazi ya uzalishaji, ahsante sana.