Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 5 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 77 2023-02-06

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza:-

Je, ni kwa kiwango gani task forces zimepunguza tatizo la uvuvi haramu katika Ziwa Victoria kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Oscar Ishengoma Kikoyo, Mbunge wa Muleba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha miaka mitatu kuanzia mwaka 2017/2018 - 2019/2020, Kikosi Kazi kilifanya doria na operesheni katika maeneo mbalimbali ya Ukanda wa Ziwa Victoria. Utekelezaji wa doria hizo uliwezesha kukamatwa kwa zana haramu zilizokuwa zikitumika katika shughuli za uvuvi ikiwemo nyavu za makila, makokoro, nyavu za timba (monofilament) na nyavu za dagaa. Pia, vifaa vilivyokuwa vinatumika kwenye uvuvi haramu na utoroshaji wa mazao ya uvuvi ikiwemo injini pamoja na boti na magari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa doria hizo katika maeneo ya Ukanda wa Ziwa Victoria uliwezesha kupungua kwa vitendo vya uvuvi haramu, biashara ya samaki wachanga na utoroshaji wa mazao ya uvuvi kwenda nje ya nchi kwa asilimia takribani 80; ahsante.