Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kusafisha maji kabla ya kusambazwa ili kuondoa Floride ambayo huleta ulemavu kwa Wakazi wa Arumeru?

Supplementary Question 1

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi hii. Naomba nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake haya, nimkumbushe tu upatikanaji wa maji ni jambo moja, lakini upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi wetu ni haki yao ya msingi na wanahitaji maji haya safi na salama muda wote.

Je, ni lini sasa Serikali itakamilisha mikakati hii ya kusafisha maji katika Wilaya ya Arumeru ili wananchi wetu waweze kupata maji safi na salama? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; kwa kuwa madhara ya madini haya ya fluoride ni makubwa sana kwa wananchi wetu yanayopelekea kupata udumavu na ulemavu.

Je, Serikali haioni sasa haja ya kuanzisha program maalum kwa ajili ya kuwatibu wananchi hawa? Ahsante (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zaytun Swai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nipokee pongezi zake, lakini vilevile naye nimpongeze kwa namna ambavyo ni mfuatiliaji mzuri na kwa sababu ni mama ndiyo maana anaongelea hata masuala ya ulemavu kwa watoto kwa sababu ni kweli watoto wanaathirika na watu wazima pia. Kama Wizara tunaendelea na utaratibu wa kuona namna njema ya kuwa sehemu ya kuwafariji hawa walioathirika na madini ya fluoride.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la lini mradi huu utakamilika. Tayari mradi upo katika utekelezaji, mradi mkubwa ambao utaleta maji katika maeneo yote ambayo yameathirika. Sasa hivi tunatarajia tu mgao ujao wa fedha tuendelee kuleta fedha katika Jimbo la Arumeru.

Name

Nancy Hassan Nyalusi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kusafisha maji kabla ya kusambazwa ili kuondoa Floride ambayo huleta ulemavu kwa Wakazi wa Arumeru?

Supplementary Question 2

MHE. NANCY H. NYALUSI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante; je, ni lini Serikali itajenga mtambo wa kusafisha na kutibu maji katika Chanzo cha Mgombezi - Ilula?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nyalusi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Chanzo cha Mgombezi ni moja ya vyanzo muhimu sana katika eneo la Iringa. Katika mwaka ujao wa fedha tuna mradi mkubwa sana wa USD Million 88.4. Kupitia mradi huu tunatarajia chanzo kile pia kiwe sehemui ya wanufaika kwa kupata eneo la treatment plant, lakini vilevile maeneo ya Kilolo pia yatapata kunufaika na tunatarajia pia kuwa na uboreshaji wa huduma ya maji safi na maji taka katika eneo la Iringa.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kusafisha maji kabla ya kusambazwa ili kuondoa Floride ambayo huleta ulemavu kwa Wakazi wa Arumeru?

Supplementary Question 3

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa kutibu maji ni gharama sana ili yafikie hatua ya kuwa maji safi na salama na wananchi kuyatumia kwa uhakika, lakini maji hayo hayo yanayogharamiwa sana na Mamlaka za Maji na RUWASA na wote ambao na Wizara pia yanatumika kuonyeshea magari, yanatumika kwenye kuzima moto, yanatumika kwenye kufrashi vyoo.

Je, ni lini sasa Serikali hii ya Tanzania italeta mpango mzuri wa kutumia maji safi na salama kwa ajili ya wananchi na maji hayo mengine kwa ajili ya takataka? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shally Raymond, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa Wizara ni kuhakikisha maji yote ambayo yanatumia gharama kubwa katika kuyatibu yaweze kutumika kwa matumizi sahihi ya majumbani na kwa kazi kama alizozitaja za uoshaji wa magari, tayari Wizara tuna mpango wa kuona kwamba raw water, maji ambayo bado hayajatibika yaweze kutumika.

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kusafisha maji kabla ya kusambazwa ili kuondoa Floride ambayo huleta ulemavu kwa Wakazi wa Arumeru?

Supplementary Question 4

MHE. MWANTUM M. ZODO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Wananchi wa Wilaya ya Handeni Mjini wanapata maji kutoka kwenye Kisima cha Nderema ambao ni Mradi wa Serikali, tunaishukuru sana Serikali. Hata hivyo, kisima hicho maji yake yana chumvi sana, je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha wanaenda kuchuja maji yale ili yawe maji safi na salama?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zodo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kisima chochote ambacho kimechimbwa na maji yake bado yana tope Serikali kupitia Wizara tumeendelea na mipango madhubuti ya kuhakikisha tunapata treatment plant kwenye maeneo hayo, hivyo Mheshimiwa Mbunge, pamoja na hiki kisima ulichokitaja na chenyewe kipo kwenye Mpango wa kuweza kujengewa treatment plant. (Makofi)