Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 5 Water and Irrigation Wizara ya Maji 76 2023-02-06

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kusafisha maji kabla ya kusambazwa ili kuondoa Floride ambayo huleta ulemavu kwa Wakazi wa Arumeru?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zaytun Seif Swai, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kutekeleza mikakati ya kuondoa madini ya fluoride kwenye maji ya kunywa na kupikia katika maeneo mbalimbali yaliyoathirika na madini hayo. Mikakati hiyo ni pamoja na kujenga Miradi ya Kusambaza Maji Safi na Salama kutoka kwenye vyanzo vya maji vya uhakika ambavyo havijaathirika na madini ya fluoride; kusambaza teknolojia ya kuondoa madini ya fluoride kwa kutumia chengachenga za mkaa wa mifupa ya ng’ombe; na kuweka mitambo ya reverse osmosis kwa ajili ya kusafisha maji ikiwa ni pamoja na kuondoa madini ya fluoride kwenye maji ya kunywa na kupikia katika Kata za Oldonyosambu, Ngaramtoni, Embasenyi katika Wilaya za Arumeru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, Wizara kupitia Kituo cha Utafiti cha Kuondoa Madini ya Fluoride cha Ngurdoto imeendelea kutoa elimu kuhusu madhara ya kiwango kikubwa cha madini ya fluoride katika maji ya kunywa na matumizi sahihi ya teknolojia ya kuondoa madini hayo kupitia vyombo vya habari, mikutano na makongamano mbalimbali.