Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: - Je, ni lini Minara yenye Kasi Kubwa itajengwa Kata za Nhwande, Kanoge, Uyowa, Silambo, Makingi, Ichemba, Igombemkulu na Mwongozo?

Supplementary Question 1

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Mwenyekiti nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali linguine la nyongeza. Pamoja na mjibu mazuri ya serikali lakini nina maswali ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajua kabisa minara ya simu au huduma za simu zinafanywa kibiashara, na mwananchi anaponunua vocha yake au internet anadhamiria apate huduma kulingana na pesa aliyoweka. Hata hivyo, cha ajabu kutokana na kasi ndogo ya hii minara au hizi huduma za simu, wananchi wanafikia mwisho wa muda wa kutumia ile fedha yake ilhali hajapata huduma aliyokusudia. Sasa swali langu: -

Je, kwa kuwa hizi fedha za hawa wananchi wangu zinazokuwa zimetumika ilhali hawajapata huduma, je hizi kampuni za simu ziko tayari kuwafidia hao wananchi wetu ambao pesa zao zimetumika bila kupata huduma kwa sababu inaonekana huu ni wizi kama wizi mwingine?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Rehema Juma Migilla Mbunge wa Ulyankulu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa labda niseme kuwa minara amabayo imejengwa katika hizi kata 4 ambapo Mheshimiwa Mbunge ameonesha kulalamikia huduma inayotolewa pale, inatoa huduma ya 2G peke yake, haijaanza kutoa huduma ya 3G. Sasa mpango wa Serikali ni kuhakikisha kwamba tunaenda ku-upgrade minara hii amabyo ilikuwa inatoa huduma ya 2G kwenda kwenye 3G, ambapo tukishafikia kwenye 3G na 4G maana yake kwamba Mtanzania na mwananchi wa Ulyankulu ataweza kutumia huduma ya internet bila kuwa na changamoto yoyote ile, ahsante.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: - Je, ni lini Minara yenye Kasi Kubwa itajengwa Kata za Nhwande, Kanoge, Uyowa, Silambo, Makingi, Ichemba, Igombemkulu na Mwongozo?

Supplementary Question 2

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Nakushukuru Mheshimiwa Mwenyekiti kata ya Masisiwe haijawahi kuwa na mnara wala mawasiliano tangu uhuru wa nchi yetu.

Je, ni lini Serikali itajenga mnara katika kata hiyo ili wananchi waweze kupata mawasiliano?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Kilolo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti ya mwaka 2021/2022 Serikali ilileta vijiji ambavyo vinaenda kupatiwa mawasiliano ikiwemo kata ya Masisiwe. Mheshimiwa Mbunge tayari tushawasiliana na iliingizwa kwenye mradi wa Tanzania ya Kidigitali, mradi amabao umefunguliwa tarehe 31 Januari, 2023. Hivyo basi mchakato wa tenda utakapokamilika tutajua kwamba ni mtoa huduma gani ambaye amepatikana kwa ajili ya kufikisha mawasiliano katika kata ya Masisiwe.

Mheshimiwa mwenyekiti, ahsante.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: - Je, ni lini Minara yenye Kasi Kubwa itajengwa Kata za Nhwande, Kanoge, Uyowa, Silambo, Makingi, Ichemba, Igombemkulu na Mwongozo?

Supplementary Question 3

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kata ya Tumbakose na kata ya Kimaha mawasiliano ni hafifu sana, naomba kujua commitment ya Serikali kwenda kujenga mnara maeneo hayo. Ahsante.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Monni, Mbunge wa Chemba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo ambayo hayana kabisa huduma ya mawasiliano tunatumia Sheria yetu Namba 11 ya mwaka 2006 iliyoanzisha Mfuko wa Mawasiliano kwa wote kwenda kufikisha mawasiliano kwenye eneo hilo. Lakini kama mawasiliano ni hafifu na kuna changamoto ya ubora wa mawasiliano kwa Sheria yetu Namba 12 ya mwaka 2003 iliyoanzisha Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, tunaielekeza Mamlaka ya Mawasiliano TCRA iende ikapime ubora wa mawsiliano ili tujiridhishe changamoto ipo wapi, ili tuhakikishe kwamba wananchi wa Chemba wanapata mawasiliano ya hakika na ubora unaotakiwa, ahsante.

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: - Je, ni lini Minara yenye Kasi Kubwa itajengwa Kata za Nhwande, Kanoge, Uyowa, Silambo, Makingi, Ichemba, Igombemkulu na Mwongozo?

Supplementary Question 4

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipatia nafasi. Katika Jimbo la Newala Vijijini kuna changamoto kubwa ya mawasiliano hasa katika kata za Chitekete, Makukwe na baadhi ya vijiji vya Nambali na Mkomatu.

Je, ni lini Serikali italeta mawasiliano katika maeneo husika?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna, Mbunge wa Newala Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa jimbo la Newala Vijijini lina changamoto, na mimi nilishafika kule; lakini Jimbo hili baadhi ya kata tuliziingiza katika utekelezaji wa miradi wa Special Zones and Border,s lakini vile vile baadhi ya kata tumeziingiza kwenye Mradi wa Tanzania ya Kidigitali. Pamoja na hayo yote Mheshimiwa Waziri pia amepanga timu moja ya kuzunguka na kujiridhisha katika maeneo ambayo yana changamoto kubwa ili tuyapatie kipaumbele, tunaamini kwamba timu hiyo itakapoleta majibu ya tathmini Waheshimiwa Wabunge tutaweza kuwahudumia kwa sababu ni dhamira ya Serikali ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuhakikisha kwamba Watanzania wote wanapata huduma ya mawasiliano, ahsante.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: - Je, ni lini Minara yenye Kasi Kubwa itajengwa Kata za Nhwande, Kanoge, Uyowa, Silambo, Makingi, Ichemba, Igombemkulu na Mwongozo?

Supplementary Question 5

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi ya swali la nyongeza. Katika Jimbo la Kilwa Kusini Kata za Kikole, Kata za Kiranjeranje hususani Kijiji cha Makangaga, Kata ya Nanjilinji hususani Kijiji cha Nakiu na Kata ya Lihimalyao hususani Kijji cha Mangisani na Kisongo hakuna kabisa mawasiliano. Je, ni nini mpango wa Serikali kwenda kujenga minara kwa ajili ya mawasiliano katika maeneo hayo? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Kilwa Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali dhamira yake ni kuhakikisha kwamba inatekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya Mwaka 2020 – 2025. Sisi kama Serikali maeneo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyataja naomba niyapokee ili twende tukayatazame kwa upana, tutume Timu Maalum ikafanye utafiti na tathmini ili tujiridhishe kwamba tatizo kubwa ni mawasiliano hafifu au hakuna kabisa ili tuweze kuona kwamba ni njia ipi itaenda kutatua tatizo hili, ahsante sana.