Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 5 Works, Transport and Communication Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 75 2023-02-06

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: -

Je, ni lini Minara yenye Kasi Kubwa itajengwa Kata za Nhwande, Kanoge, Uyowa, Silambo, Makingi, Ichemba, Igombemkulu na Mwongozo?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya waziri wa Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Babari, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rehema Juma Migilla Mbunge wa Ulyankulu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imetekeleza miradi ya kufikisha huduma za mawasiliano katika Kata tano ambazo ni Kata ya Kanoge, ambapo kuna mnara wa Airtel umejengwa katika eneo la Ulanga, Uyowa katika eneo la Uhindi, Ichemba eneo la Ichemba yenyewe, Igombemkulu katika eneo la Imara na Mwongozo katika eneo la Mwanditi ambapo minara hii imekamilika na inatoa huduma ya mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Minara ya Kata za Kanoge, Ichemba, Igombemkulu na Mwongozo inatumia teknolojia ya 2G/3G hivyo inatoa huduma za mawasiliano yenye kasi kubwa; na mnara huu uliopo Kata ya Uyowa unatumia teknolojia ya 2G pekee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kata ya Uyowa imengizwa kwenye mpango wa kuboreshewa huduma za mawasiliano yenye kasi na zabuni yake itatangazwa katika awamu ijayo kulingana na upatinaji wa fedha. Aidha, Serikali itafanya tathmini ya upatikanaji wa huduma za mawasiliano ya simu yenye kasi kubwa katika Kata za Nhwande, Silambo, na Makingi katika mwaka wa fedha 2023/2024, ahsante.