Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati Mahakama ya Wilaya ya Lushoto?

Supplementary Question 1

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa mwenyekiti, nakushukuru, pia namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa majibu mazuri. Nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Lushoto lina Mahakama za mwanzo mbili, kwa maana Mahakama ya Mlola na Mahakama ya Gare. Lakini hii ya Gare takribani miaka 20 sasa haifanyi kazi yani jengo lake limekeuwa ni gofu.

Je, Serikali in ampango gani wa kujenga upya Mahakama ya Gare pamoja na kata jirani ili waweze kupata huduma?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshmimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Shekilindi kama ifuatavyo: -

Mheshmimiwa Mwenyekiti, kimsingi Mahakama ya Tanzania katika mpango wake inajenga Mahakama za Mwanzo katika Makau Makuu ya Tarafa zote hapa nchini.

Kata ya Gare haipo kama sehemu ya Makao Makuu ya kata kwa sababu iko ndani ya Tarafa ya Lushoto yenyewe. Hivyo tunaangalia uwezekano wa kuzipa umuhimu kata ambazo zina uhitaji maalum. Baada ya Bunge hili tutawasiliana na Mheshimiwa Mbunge kujua uhalisia wa tatizo la Gare lakini kwa sasa tunaelekeza nguvu zetu Makao Makuu ya Tarafa hapa nchini.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati Mahakama ya Wilaya ya Lushoto?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati Mahakama ya Mwanzo ya Mbagala ambayo ina hali ngumu sana, mazingira yake na idadi ya watu wanaopata huduma pale ni wengi sana?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi tumelichukua ombi lake na tutakwenda kulifanyia kazi ili tuweze kuiweka katika mazingira mazuri ya matumizi, ahsante.