Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 5 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 74 2023-02-06

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati Mahakama ya Wilaya ya Lushoto?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshmimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shabani Omari Shekilindi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mahakama ya Tanzania inaendelea kutekeleza kwa awamu Ujenzi na ukarabati wa majengo yake sehemu mbalimbali hapa nchini. Katika mpango huu, yapo majengo ambayo yanahitaji kujengwa upya kutokana na hali yake na ufinyu wa jengo ikilinganishwa na mahitaji ya sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kulingana na hali ya jengo la Mahakama ya Wilaya ya Lushoto, imeamuliwa kuwa jengo hili lijengwe upya badala ya kukarabatiwa lile jengo lililopo kwani ni la zamani sana, finyu na baadhi ya miundombinu yake hairuhusu ukarabati mkubwa. Hivyo, kulingana na Mpango, jengo jipya la Mahakama ya Wilaya ya Lushoto litajengwa kwenye kipindi cha fedha 2024/2025. Aidha, kwa sasa jengo lililopo litaendelea kufanyiwa matengenezo madogo madogo hadi litakapopatikana jengo jipya.