Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: - Je, ni lini wastaafu wa ATCL watalipwa mafao yao?

Supplementary Question 1

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali ya nyongeza. Kwanza nampongeza kwa jibu lake zuri ambalo linaridhisha. Swali langu la kwanza; kwa kuwa deni hilo la wastaafu lilirithiwa kabla ya mpango maalum wa kufufua ATCL, nilitaka kujua sasa hivi Serikali ina mpango gani wa kuzuia kuzalisha madeni mengine mapya?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, kwa kuwa Serikali imejikita zaidi katika kutoa mafunzo mbalimbali katika vyuo vyake ikiwepo Chuo cha Usafirishaji, nilitaka kujua hadi sasa tuna marubani wangapi wazalendo ambao wako katika ndege zetu za ATCL? Ahsante.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nami niweze kujibu maswali mawili ya nyongeza, ya Mheshimiwa Angelina Adam Malembeka, Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia masuala haya ya ATCL.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza anataka kujua mpango wa kuzuia madeni mapya baada ya kuanza mpango ule wa ufufuaji wa kampuni hii yetu ya ndege nchini. Serikali imejipanga kuzuia ama kutozalisha madeni mengine. Hadi sasa tangu mwaka 2016 tumekuwa tukilipa wafanyakazi wote na hakuna deni jipya; lakini kwenye mwaka wa fedha huu 2022/2023 ambao tunaendelea nao tumetenga takribani kiasi cha shilingi bilioni 10 ili kulipa wafanyakazi wote waliokuwa wa ATCL kama deni la nyuma.

Mhehsimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili anataka kujua idadi ya marubani tulio nao hapa nchini hususan wanawake na wanaume. Tuna takribani ya marubani 106. Kati ya hao marubani 11 ni wanawake na marubani 95 ni wanaume; kwa maana ya kwamba hawa wanawake wanarusha ndege zote kwa sababu hapa nchini tuna ndege aina tatu ambapo tuna Dash 8Q400, Bombardier al maarufu Bombadier ama sasa hivi inaitwa DeHaveland lakini pia tuna Airbus 220-300 ambapo pia wanawake wanarusha na tuna Boeing 787-8 ambayo pia wanawake wanarusha hizi ndege. Na kati ya hao 106. 105 wote ni watanzania, ni mmoja tu ambaye sio Mtanzania.