Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 5 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 73 2023-02-06

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: -

Je, ni lini wastaafu wa ATCL watalipwa mafao yao?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Angelina Malembeka Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kabla ya kuanza kwa juhudi za ufufuaji wa ATCL Septemba 2016, ATCL ilikuwa ikikabiliwa na changamoto za uendeshaji kwa kukosa mtaji, kuwa na ndege mbovu, kushindwa kulipa madeni ya wazabuni na kutowasilisha michango ya wafanyakazi katika mifuko ya hifadhi ya jamii. Aidha, baada ya mwaka 2016, ATCL imekuwa ikiwasilisha michango ya wafanyakazi kwenye mifuko ya jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuzingatia uhakiki uliofanyika, ATCL ina madeni ya jumla Shilingi 4,864,673,387.85 yanayotokana na kutowasilisha michango ya wanyakazi kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii. Fedha za kulipa madeni hayo zimetengwa katika bajeti ya mwaka 2022/2023. Hivyo, madeni hayo ya michango ya wafanyakazi kwenye mifuko ya jamii yatalipwa katika mwaka huu wa fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.