Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kiwanja cha Ndege katika Mkoa wa Manyara?

Supplementary Question 1

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Nina maswali madogo ya nyongeza. Kwanza naipongeza Serikali kwa hatua hiyo, sasa tunaelekea kwenye upembuzi yakinifu pamoja na usanifu. Sasa hamu ya wana Manyara ni kuwa na kiwanja cha ndege. Sasa Serikali imejipangaje kukamilisha hatua hiyo ya usanifu?

Swali langu la pili, je, Serikali ina mpango gani sasa wa kufidia wananchi ambao maeneo yao yatatwaliwa kwa ajili ya ujenzi wa kiwanja cha ndege baada ya kukamilisha uthamini huo? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Yustina Arcadius Rahhi, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeshaanza, kama nilivyosema, tumeshatafuta mhandisi elekezi kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina; na huyo ndie atakayetupa sasa gharama halisi ya fidia. Baada ya hapo Serikali basi itatafuta fedha ili kabla hatujaanza ujenzi tuwafidie hao wananchi amabo watapisha ujenzi wa eneo hilo, ahsante.