Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 5 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 72 2023-02-06

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kiwanja cha Ndege katika Mkoa wa Manyara?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yustina Arcadius Rahhi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na utaratibu wa kutwaa eneo kwa ajili ya ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Mkoa wa Manyara.

Mheshmiwa Mwenyekiti, hadi sasa Serikali imeshamaliza kuandaa hadidu za rejea kwa ajili ya kumpata mhandisi elekezi atakayefanya upembuzi yakinifu pamoja na usanifu wa kina ili kubaini gharama za ujenzi. Hivyo, ujenzi wa kiwanja hicho utaanza baada ya usanifu kukamilika, ahsante.