Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuwawezesha wachimbaji wadogo wanawake kwa kuwapa mikopo?

Supplementary Question 1

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali moja dogo la nyongeza lenye sehemu (a) na (b) kama ifutavyo: -

(a) Je, Mhesnimiwa Naibu Waziri, anaweza kunieleza ni vikundi vingapi na kwa kiasi gani vya wanawake wa Mkoa wa Ruvuma wamekopeshwa fedha hizo?

(b) Serikali ina mpango gani wa kutumia survey data ili kuwa ni dhamana ya kuweza kuwakopesha hao wachimbaji wadogo wadogo kwa sababu wachimbaji wengi hawana dhamana ya kuweka kwenye mikopo yao? Ahsante.

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili madogo au swali moja lenye kipengele (a) na (b) la Mheshimiwa Jacqueline Msongozi, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Ruvuma kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa idadi ya waliokopeshwa kutoka Mkoa wake, hatujaweka mchanganuo wa kimkoa lakini kwa ujumla wakiweko wachimbaji wadogo wanawake na wanaume hadi sasa zaidi ya vikundi na wachimbaji wadogo 110 wameshafikiwa na mikopo kutoka mabenki ya ndani ambayo yamekubali kukopesha wachimbaji waliokidhi vigezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa swali lake la pili kuhusu data za jiolojia kutumika kama dhamana ya kupata mikopo ya benki, kama nilivyojibu kwenye swali la msingi ni kwamba, tutakapokuwa tumepata hivi vifaa vya kuwasaidia wachimbaji wadogo kwenye utafiti, data zile sasa zitatumika kama mojawapo ya vigezo ikiwepo pia wao kuweka kumbukumbu za uchimbaji wao, ndiyo maana hata waliofanikiwa kufanya hivyo hadi sasa, watu 110 walio kwenye mnyororo wa thamani wa madini wameshakopeshwa zaidi ya Bilioni 80 na Benki ya NMB na Benki ya CRDB pia imeshawakopesha kiasi cha Bilioni 65. Kwa hiyo, Bilioni 145 zimeshawasaidia wachimbaji waliojipanga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutoa wito kwa wanavikundi walioko katika Mkoa wake nao wajipange, waweke taarifa zao sahihi na mitambo hii ikija tutafanya utafiti na wataweza kutumia kama moja ya vigezo. Ahsante.

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuwawezesha wachimbaji wadogo wanawake kwa kuwapa mikopo?

Supplementary Question 2

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, Serikali pamoja na kuwa imeweka utaratibu wa kutoa mikopo kupitia taasisi za kifedha, lakini mikopo hii imekuwa na masharti magumu amabyo wachimbaji wetu wadogo wengi wameshindwa kuweza kuyafikia.

Je, Serikali haioni haja sasa ya kupunguza masharti na ikiwezekana iweze kutoa ruzuku kwa wachimbaji wadogo ili tuweze kuwasaidia katika uchumi wa madini.

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kasaka, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, masharti ya kibenki yanaonekana kuwa ni magumu kwa sababu wachimbaji wadogo hawajapata uelewa mzuri wa namna ya kujipanga kupata mikopo hii. Kazi yetu kama Wizara imekuwa ni kutoa elimu ya vigezo muhimu ambavyo wanatakiwa wazingatie ili waweze kukopeshwa au waweze kukopesheka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo Wizara tutaendelea kujadiliana na mabenki na kuona namna ya kutengeneza masharti rafiki na rahisi kueleweka ili wachimbaji hawa waweze kupata mikopo bila usumbufu. (Makofi)

Mheshimiwa Sophia Mwakagenda, swali la nyongeza.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuwawezesha wachimbaji wadogo wanawake kwa kuwapa mikopo?

Supplementary Question 3

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na wanawake hawa kupata mikopo kuna shida kubwa sana kwenye biashara ya madini wanawake kupata masoko. Serikali ina mpango gani wa kujipanga kuhakikisha wanawake hawa pamoja na kwamba wanapewa mikopo lakini pia watafutiwe masoko ili bishara zao ziende vizuri?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwakagenda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti suala la masoko sio issue tena nchini kwetu baada ya Wizara kuanzisha masoko ya madini na vituo vya kununua madini nchini. Kwa sasa tuna zaidi ya masoko 47 na vituo 84 na bei elekezi hutolewa na Wizara kila wakati na kwa madini ya dhahabu bei ya dunia hutumika katika kuwapa bei stahiki.