Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 5 Energy and Minerals Wizara ya Madini 71 2023-02-06

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuwawezesha wachimbaji wadogo wanawake kwa kuwapa mikopo?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jacqueline Ngonyani Msongozi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhakikisha wachimbaji wadogo hususan wanawake wanapata mikopo, Serikali kupitia STAMICO imepanga kununua mitambo mitano (5) midogo ya uchorongaji (utafiti madini) ambapo taratibu za ununuzi wa mitambo hii zinakamilishwa hivi sasa. Mitambo hiyo itawazesha wachimbaji wadogo kujua kiasi cha mashapo yaliyopo katika maeneo yao. Aidha, STAMICO imeingia makubaliano ya ushirikiano (MoU) na baadhi ya mabenki nchini kutoa mikopo kwa wachimbaji wadogo wakiwemo wanawake. Benki hizo ni CRDB, NMB na KCB ambapo katika utekelezaji wa makubaliano hayo, benki hizo zimejengewa uelewa wa sekta ya madini na namna nzuri ya utoaji mikopo kwa sekta hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Madini imekuwa ikiwahamasisha wachimbaji wadogo hususan wanawake kujiunga katika vikundi ili kurahisisha utoaji huduma mbalimbali zinazolenga kuwawezesha kupata fedha, vifaa vya uchimbaji na uchenjuaji wa madini. Ahsante sana.