Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kushughulikia huduma za afya kwa uchunguzi tiba na kujikinga katika Shule za Msingi na Sekondari?

Supplementary Question 1

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa majibu ya Serikali.

Kwa kuwa mchakato wa bima ya afya kwa wote umo mbioni kukamilishwa, na kwa kuwa miaka ya nyuma kulikuwa na utaratibu mzuri wa kwenda kuchunguza afya za watoto mashuleni kwa vipindi kadhaa kwa mwaka. Je, Serikali haioni umuhimu wa kurudisha mpango huu wa kuchunguza afya za vijana wetu shuleni walau mara mbili kwa mwaka, katika jitihada za kupunguza gharama kwa kugundua maradhi mapema ili kukinga na kuwapunguzia wanafunzi hawa shida au wazazi wao kupeleka hospitali wanapokutwa maradhi yameshawatokea?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asha Abdullah Juma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli ni muhimu sana kuwa na utaratibu wa ku-check afya za wanafunzi shuleni angalau mara mbili kwa mwaka, utaratibu huo uko kwenye miongozo yetu, ni kweli kwamba hapa katikati ufanisi wake umepungua kidogo. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwanza tumepokea ushauri wake tutakwenda kutekeleza, pia nitoe maelekezo kwa Wakuu wa Shule na Halmshauri zetu kuhakikisha wanaweka utaratibu kwa kutumia Waratibu wa Elimu, pia na Waratibu wa Huduma za Afya katika shule ili watoto wetu wachekiwe mara kwa mara afya zao na kupewa matibabu mapema. Ahsante. (Makofi)