Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 70 2023-02-06

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kushughulikia huduma za afya kwa uchunguzi tiba na kujikinga katika Shule za Msingi na Sekondari?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asha Abdullah Juma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, huduma ya afya kinga na tiba shuleni ni afua muhimu inayotekelezwa na Serikali kuwajengea watoto uelewa wa kujikinga na magonjwa. Huduma hii inahusisha utoaji wa elimu ya afya, utambuzi wa magonjwa katika hatua ya awali pamoja na uratibu wa kupata matibabu kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Halmashauri imeendelea kuratibu utolewaji wa elimu na huduma za afya kwa watoto walioko shuleni, hususani kwenye magonjwa ya malaria, minyoo, kichocho, saratani ya mlango ya kizazi, afya ya kinywa, meno pamoja na macho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha mwaka 2021/2022, Serikali kwa kushirikiana na wadau wa afya iligawa vyandarua 3,104,401 kwenye shule za msingi 7,639 kwa uwiano wa chandarua kimoja kwa kila mtoto. Pia, chanjo ya kuzuia maambukizi ya saratani ya mlango wa kizazi ilitolewa kwa wasichana 623,501 dozi ya kwanza na 472,460 dozi ya pili. Aidha, kila mwaka hufanyika kampeni ya utoaji dawa za minyoo na matone ya vitamini ‘A shuleni, ahsante.