Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga vyumba vya kujifungulia akina Mama kwenye Zahanati za Dirma, Laghanga na Getanus?

Supplementary Question 1

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, changamoto ya ufinyu wa maeneo ya kutolea huduma ya afya ya mama na mtoto hasa eneo la kujifungulia ipo maeneo mengi ndani ya Wilaya yangu ya Hanang.

Je, sasa Serikali haioni ni wakati muafaka kufanya tathmini ya jumla wakati tukiendelea kupanga mpango wa kujenga kituo cha afya kila Kata ili kufanya maboresho katika maeneo hayo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili fedha zilizotengwa kwa zahanati ya Laghanga, milioni 10. Je, Serikali haioni kwamba hizo fedha ni kidogo haiwezi kutosheleza?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Samweli Xaday Hhayuma, Mbunge wa Jimbo la Hanang, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba zahanati zile ambazo zilijengwa miaka ya nyuma zilikuwa ndogo na vile vyumba vya kujifungulia vilikuwa finyu lakini kwa sasa Serikali imeboresha sana ramani zetu, ramani zetu ni kubwa zina vyumba vya kutosha vya kujifungua, lakini pia vya kupumzika wakina mama baada ya kujifungua. Kwa hiyo nimhakikishie kwamba kwa ramani za sasa tutajenga zahanati zenye nafasi za kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kujenga vituo vya afya kila Kata utaratibu wa Serikali tutajenga vituo vya afya vya kimkakati katika maeneo ya kimkakati ambayo yana idadi kubwa ya watu lakini umbali mkubwa kutoka kituo cha huduma cha Jirani zaidi. Lakini hii shilingi milioni 10 imetengwa kutoka mapato ya ndani na chumba kinakwenda kuongezwa katika jengo lile ambalo linatumika kwa sasa, kwa hiyo tunaamini itatosha na kama haitatosha basi Serikali itaongezea kuhakikisha kwamba chumba hicho kinakamilika. Ahsante. (Makofi)

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga vyumba vya kujifungulia akina Mama kwenye Zahanati za Dirma, Laghanga na Getanus?

Supplementary Question 2

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kituo cha afya cha Nguvukazi - Chanika kinahudumia mama na mtoto na Serikali, ni lini sasa itaona umuhimu wa kujenga majengo wezeshi kama wodi za wanawake, wanaume na chumba cha kuhifadhia maiti ili kituo cha afya hiki kipate hadhi ya kuwa Hospitali na kuwahudumia wananchi wa Kata za Chanika, Buyuni, Zingiziwa na Msongola?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jerry Silaa, Mbunge wa JImbo la Ukonga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Kituo cha Afya hiki cha Chanika kinahudumia wananchi wengi na tulishatoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam kwa maana ya Manispaa ya Ilala, kutenga fedha kati ya asilimia 60 kwa ajili ya kufanya upanuzi na ujenzi wa wodi katika kituo hiki. Kwa hiyo, nitumie fursa hii kumuelekeza Mkurugenzi kwamba hiki ni kipaumbele cha wananchi ahakikishe anatenga fedha kwenye mapato ya ndani ili tuweze kujenga wodi hizo. Ahsante. (Makofi)