Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 69 2023-02-06

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza: -

Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga vyumba vya kujifungulia akina Mama kwenye Zahanati za Dirma, Laghanga na Getanus?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Samweli Xaday Hhayuma, Mbunge wa Jimbo la Hanang, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa vituo vya kutolea huduma za afya kutoa huduma ya kujifungua, zikiwemo zahanati za Dirma, Laghanga na Getanus zilizopo Halmashauri ya Hanang. Katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali kupitia Halmashauri ya Hanang itatenga kiasi cha shilingi milioni 10 kwa ajili ya ujenzi wa chumba cha kujifungua katika jengo la Zahanati ya Laghanga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, upanuzi wa vyumba vya kujifungua katika zahanati za Dirma na Getanus utafanyika katika mwaka wa fedha 2024/2025. Ahsante.