Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, ni kiasi gani cha ngozi kinazalishwa kwa mwaka mzima na kutumika nchini na kiasi gani ghafi kinauzwa nje ya nchi?

Supplementary Question 1

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naishukuru Serikali kwa majibu mazuri: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, nchi yetu inauza ngozi ya bilioni 10 tu kwa mwaka, lakini nchi hii-hii ndiyo ambayo imebarikiwa kuwa na mifugo mingi zaidi.

Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kuongeza uzalishaji huo kwenye hivyo vituo viwili ambavyo vina-process mpaka mwisho ikiwepo Himo Tanneries na Moshi Leather Industries ili waweze kukidhi uhitaji wa nchi hii baada ya kufunguliwa kiwanda cha uzalishaji wa Kilimanjaro International Leather Industries?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Serikali ina mkakati gani kutoa elimu kwa wananchi wake ili kuhakikisha kwamba, mifugo inatoa ngozi bora na salama katika kipindi chote cha mwaka, ili kutoa ajira zaidi kwa vijana, wakiwemo vijana wa Kilimanjaro? (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Shally Raymond, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli lengo letu kama Serikali ni kuona uzalishaji kwenye viwanda vyetu vya ndani unaongezeka, jitihada kadhaa zinafanywa, ikiwemo kuondoa changamoto na kuboresha mazingira ya biashara. Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kushughulikia changamoto hizo ikiwa ni pamoja na ile ya kuondoa tozo na kodi mbalimbali zenye kuweka mkwamo wa upatikanaji wa malighafi na ushindani kwenye biashara. Baada ya kuyafanya haya tunayo imani kuwa, viwanda vyetu sasa vitapokea malighafi nyingi kutoka kwa wazalishaji ili kuviwezesha kufanyakazi yake kwa ufasaha zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili; ni mkakati gani juu ya elimu ni kwamba Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan imetenga fedha, mwaka huu tumetenga fedha kwa ajili ya kutoa elimu kwa wachunaji wa ngozi, lakini pia vilevile kununua vifaa kama computers, ili tuweze kuwa na record ya uzalishaji sahihi wa ngozi na hatimae kuwawezesha kuwaingiza katika masoko ikiwemo viwanda vyetu ambavyo vinazalisha hapa nchini, ambavyo tayari Mheshimiwa Shally Raymond ameshavitaja. Ahsante sana. (Makofi)