Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 4 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 67 2023-02-03

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: -

Je, ni kiasi gani cha ngozi kinazalishwa kwa mwaka mzima na kutumika nchini na kiasi gani ghafi kinauzwa nje ya nchi?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shally Josepha Raymond, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yetu inazalisha wastani wa vipande milioni 13.6 vya ngozi kwa mwaka. Kati ya vipande hivyo, milioni 4.2 ni vya ng’ombe, vipande milioni 6.9 ni vya mbuzi na vipande milioni 2.5 ni vya kondoo. Kwa sasa, tunavyo viwanda vitatu vinavyofanya kazi ya usindikaji wa ngozi katika hatua ya kati (wet blue) na hatua ya mwisho (finished leather).

Mheshimiwa Naibu Spika, ngozi zinazosindikwa katika hatua ya kati ni vipande 51,866 vya ngozi ya ng’ombe na vipande 262,229 vya mbuzi na kondoo. Usindikaji hadi hatua ya mwisho ni vipande 145,000 vya ngozi ya ng’ombe na vipande 259,000 vya ngozi ya mbuzi na kondoo. Pia, kuna wasindikaji wadogo wanaosindika na kutengeneza bidhaa za ngozi maeneo mbalimbali hapa nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yetu inauza nje ya nchi ngozi ghafi na iliyosindikwa hatua ya awali, wastani wa vipande 1,630,740 vyenye thamani ya Shilingi Bilioni 10.5 kwa mwaka. Ngozi hiyo, inauzwa katika nchi za Nigeria, Afrika ya Kusini, Ghana, Togo, Pakistan, Marekani, Italia, Dubai na China, ahsante sana.