Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa vibali ili kuajiri walimu na kuondoa upungufu wa walimu uliopo nchini?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante mwanzoni nilisema Spika, nafanya marekebisho. Kwa kuwa kuna upungufu mkubwa wa walimu wa hisabati, na wanafunzi wamekuwa wakishindwa kufanya vizuri kutokana na ukosefu wa walimu wa hisabati. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha shule zote nchini zinapatiwa walimu wa hisabati kama ilivyowahi kufanya kwenye somo la sayansi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Josephine Johnson Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tunatambua kuna shule hazina walimu hususani wa somo la hisabati na upungufu umekuwa mkubwa. Ndiyo maana katika mpango wetu, ambapo tumeomba kibali Utumishi, tutakapokuwa tumepata sehemu yake ni kuajiri walimu wa sayansi hususani walimu wa hisabati ili kuhakikisha kwamba tunakabiliana na hii changamoto iliyopo, ahsante sana.

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa vibali ili kuajiri walimu na kuondoa upungufu wa walimu uliopo nchini?

Supplementary Question 2

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimwa Naibu Spika, na mimi napenda kuuliza swali la nyongeza; kwa maana ya kwamba tunafahamu changamoto ya walimu wa sayansi kwenye Jimbo la Arusha Mjini ni kubwa sana na hata kwa nchi nzima. Je, Serikali ina mpango gani wa kuja na mkakati Madhubuti wa kuondoa changamoto ya walimu wa sayansi wa nchi nzima?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mrisho Gambo, Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwamba mpango wa Serikali namba moja ni kuajiri ajira mpya ambazo sehemu kubwa itakuwa ni kuchukua walimu wa sayansi. Mpango wa pili ni kuhakikisha kwamba sasa hivi sisi Ofisi ya Rais-TAMISEMI tukishirikiana na Wizara ya Elimu matarajio yetu ni kuanza kuwatumia hao walimu waliomaliza ambao watakuwa wanajitolea wenye professional hiyo kuhakikisha kwamba tunaondoa hiyo changamoto. Kwa hiyo tumejipanga vizuri kuhakikisha kwamba masomo ya sayansi tunapaa walimu na vifaa vilevile ili kuhakikisha wakati wote yanakuwa yanafundishwa, ahsante sana.