Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: - Je, ni lini Kata za Sirari na Nyamongo zitapandishwa hadhi na kuwa Mamlaka za Miji Midogo?

Supplementary Question 1

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Maeneo yote hayo mawili ya Sirari na Nyamongo ni ahadi za Viongozi Wakuu wa Serikali, sasa nimuombe Mheshimiwa Waziri kama yupo tayari majibu haya haya tuyapeleke pale Sirari na Nyamongo akayaseme mwenyewe? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, nipo tayari tuongozane na Mheshimiwa Mbunge na bahati nzuri wiki mbili zilizopita tulikuwa Tarime Vijijini tumefanya ziara pamoja na niko tayari turejee tena Tarime kwenda Sirari na Nyamongo.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: - Je, ni lini Kata za Sirari na Nyamongo zitapandishwa hadhi na kuwa Mamlaka za Miji Midogo?

Supplementary Question 2

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Katika Miji Midogo iliyoko nchini sasa hivi kumekuwa kuna sintofahamu kati ya Mamlaka ya Miji Midogo na Halmashauri kuhusu nani hasa akusanye mapato yapi? Je, Serikali sasa iko tayari kutoa mwongozo unaoeleweka ili mamlaka zote mbili zijue mipaka yake?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecilia Paresso, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimejibu kwenye swali la msingi tuna mamlaka za Miji Midogo 71 kote nchini inawajibika katika Halmashauri Mama na inatekeleza majukumu yake chini ya usimamizi wa Halmashauri Mama. Kwa hiyo, haina mamlaka ya moja kwa moja mpaka pale itakapopata sifa ya kuwa Halmashauri ya Mji. Kwa hiyo, ikiwa Mamlaka ya Mji mdogo bado haina mamlaka ya moja kwa moja na wao siyo Accounting Officers, kwa hiyo tutaendelea kuhakikisha kwamba kwanza tunawawezesha kwa kuwajengea uwezo lakini ku-harmonize mahusiano kati ya Halmashauri Mama lakini na Mamlaka za Mji Mdogo. Ahsante.