Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 52 2023-02-03

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: -

Je, ni lini Kata za Sirari na Nyamongo zitapandishwa hadhi na kuwa Mamlaka za Miji Midogo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwita Mwikwabe Waitara Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mpaka kufikia mwezi Januari, 2023, nchi yetu ina jumla ya Halmashauri za Miji 21 na Mamlaka za Miji Midogo 71.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa mwongozo wa uanzishaji wa mamlaka za Serikali za Mitaa wa mwaka 2014, utaratibu wa kuomba kuanzisha Mamlaka za Miji Midogo huanza na mikutano ya kujadili. Mikutano hiyo hufanywa katika ngazi ya vijiji, kisha Kamati ya ushauri ya Wilaya (DCC), Kamati ya ushauri ya Mkoa (RCC) na kuwasilishwa Ofisi ya Rais - TAMISEMI.

Mheshimiwa Naibu Spika, kusudio la kuanzisha Mamlaka za Miji Midogo katika Kata za Sirari na Nyamongo mchakato wake uliishia kwenye Kamati ya Ushauri ya Wilaya kwa kikao kilichofanyika mwaka wa fedha 2011/2012. Hivyo, Halmashauri inashauriwa kutimiza matakwa ya mwongozo.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, mpango wa Serikali kwa sasa ni kukamilisha kwanza miundombinu kwa mamlaka zilizopo kabla ya kuanzisha mamlaka mpya. Ahsante.