Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itazigawa upya Halmashauri nchini ili Wananchi wapate huduma kwa urahisi kutokana na jiografia za Halmashauri hizo?

Supplementary Question 1

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kujibu maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, baadhi ya Halmashauri zimekuwa kubwa mno na nyingine zimekuwa zina maeneo makubwa sana kijiografia, lakini nyingine zina Majimbo matatu, nyingine zina Majimbo mawili na kupata huduma wanapata katikati ambako ni Mjini.

(i) Je, serikali sasa haioni haja ya kufuata uhalisia na urahisi wa kupata huduma katika ugawaji wa Halmashauri hizo?

(ii) Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba katika utengaji wa fedha za maendeleo jiografia za Halmashauri zetu iwe ni mojawapo ya kigezo cha kuzingatiwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali wawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Grace Victor Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba tuna Halmashauri ambazo zina maeneo makubwa kijiografia, lakini kuna Halmashauri ambazo zina Majimbo zaidi ya moja na ni kweli kuna changamoto ya umbali kutoka baadhi ya maeneo ya Halmashauri kufika kwenye Makao Makuu ya Halmashauri hizo. Serikali kwa sasa sote ni mashahidi kwamba mamlaka nyingi zimeanzishwa hazina majengo muhimu ya utawala, hazina miundombinu muhimu ya huduma za jamii. Kwa hiyo, kipaumbele cha Serikali kwa sasa ni kukamilisha kweye mamlaka zilizopo na baada ya hapo taratibu zitafuatwa ili kupata mamlaka nyingine na kusogeza huduma kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili; Serikali imekuwa ikipeleka fedha kwa kuzingatia jiografia kwa maana ukubwa wa maeneo, ndiyo maana hata kwenye Mfuko wa Jimbo, kigezo mojawapo ni ukubwa wa eneo la Halmashauri husika lakini hata kwenye fedha za barabra kwa maana ya TARURA kigezo mojawapo ni hicho. Kwa hiyo, Serikali inazingatia pia ukubwa wa kijiografia wa maeneo husika. Ahsante. (Makofi)