Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 50 2023-02-03

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itazigawa upya Halmashauri nchini ili Wananchi wapate huduma kwa urahisi kutokana na jiografia za Halmashauri hizo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Grace Victor Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa ikigawa maeneo mapya ua Utawala zikiwemo Halmashauri kwa lengo la kusogeza huduma kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, mpaka sasa, Serikali inaendelea na ujenzi wa miundombinu ya huduma na kiutawala katika mamlaka mpya ambazo hazina miundombinu hiyo muhimu ili kuziwezesha kutoa huduma bora kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, mpaka sasa jumla ya majengo ya utawala 109 yenye thamani ya shilingi bilioni 356.8 yanaendelea kujengwa kote nchini, lengo la Serikali kwa sasa ni kukamilisha miundombinu katika mamlaka zilizopo kabla ya kuanzisha mamlaka mpya, ahsante.