Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, nini kauli ya Serikali kuhusu majengo yaliyopo maeneo ya Mkoa wa Dar es Salaam ambayo ujenzi wake umesimama kwa muda mrefu?

Supplementary Question 1

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Spika, ahsante, nimepokea majibu ya Serikali lakini sheria ilivyo sasa inaelekeza kwamba ujenzi au uendelezaji uanze ndani ya miaka mitatu lakini sheria hiyo haitoi ukomo ni lini majengo hayo yamalizike kujengwa. Je, Serikali haioni sasa ni wakati wa kuleta sheria ambayo itaweka ukomo katika uendelezaji wa majengo na wale ambao watakaidi waweze kupata adhabu kwa kuchelewesha ujenzi?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pil, ni nini kauli ya Serikali hasa katika uendelezaji wa majengo ya miradi ya taasisi za umma kama vile NSSF, PSSSF na National Housing ikiwemo suala la majengo yale ambayo yametelekezwa kama vile Hotel Embassy, Motel Ajib kule Dar es Salaam na mengineyo?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Tarimba Abbas kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na sheria inazungumza vipi juu ya yale majengo ambayo hayajaendelezwa; kwanza nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ndani ya sheria ya Ardhi inayohusu uendelezaji, inamtaka muendelezaji au mtu anayepewa milki aendeleze ndani ya miaka mitatu, ni kweli lakini wako baadhi ya watu wamekuwa wanafanya kazi ya kuanzisha ujenzi ndani ya miaka mitatu na kwa sababu sheria hiyo imetoa ombwe katika lini anatakiwa amalize.

Mheshimiwa Spika, ushauri wako ulioutoa tunauchukua Mheshimiwa Mbunge na ndani ya Wizara tumeendelea kufanyia kazi na itakapofika punde tutakuja kuwasilisha mbele ya Bunge lako ili Waheshimiwa Wabunge, wapate kujua sasa ni kipande gani au mwaka gani mtu anatakiwa kumaliza.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, juu ya Serikali inaendelezaje majengo yaliyosimama, maelekezo ya Serikali ni kwamba majengo yote ambayo hayajaendelezwa yaendelezwe ili yaweze kukamilika yasije yakatumika kwa matumizi yasiyofaa. Juu ya Shirika la National Housing, hasa in particular, Serikali imekwishaelekeza juu ya shirika hilo liweze kukopa na mwanzo lilikopa shilingi bilioni 44.7 kwa ajili ya uendelezaji na sasa tupo katika mazungumzo na wenzetu wa Hazina ili tuweze kukopa katika kipande kilichobakia ili tuweze kumalizia sehemu iliyobakia katika majengo mengine.