Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Suleiman Haroub Suleiman

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. SULEIMAN HAROUB SULEIMAN aliuliza: - Je, ni kwa kiasi gani Taasisi za Serikali ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zinashirikiana katika shughuli za kiuchumi?

Supplementary Question 1

MHE. SULEIMAN HAROUB SULEIMAN: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, pamoja na majawabu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza ni lini miradi ambayo inahusiana na mabadiliko ya tabia nchi iliyopo Zanzibar SMT wataimaliza? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili, Zanzibar inashirikishwa vipi kwenye mikutano ya Kimataifa hasa inayohusu masuala ya tabia ya nchi? Ahsante. (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Suleiman, Mbunge Mwakilishi kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ipo miradi mingi ambayo inatekelezwa ama inasimamaiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na inatekelezwa Zanzibar. Kuna miradi ile ambayo inasimamiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais lakini kuna miradi inayosimiamiwa na NEMC. Kwa mfano, kuna Mradi wa Adaptation Fund ambayo ipo Zanzibar na imetekelezwa maeneo tofauti. Hii tayari imeshakamilika na wananchi wameshaanza kunufaika na miradi hiyo.

Mheshimiwa Spika, pia kuna miradi ya EBA ambayo hivi karibuni kama mnakumbuka tuliwahi kukabidhi boti za uvuvi Tumbatu na Mheshimiwa Rais wa Zanzibar, lengo na madhumuni Serikali ya Jamhuri ya Tanzania inaunga mkono juhudi za Uchumi wa Bluu kwa upande wa Zanzibar na suala nzima la uhifadhi na utunzaji wa mazingira.

Mheshimiwa Spika, vile vile kuna miradi ya LSDF. Hii ni miradi ambayo imekuja kwa ajili ya kukuza kilimo, kuboresha ardhi iliyoathirika na athari za mabadiliko ya tabia nchi. Pia kuna miradi ambayo haijakamilika; hii tumeshatoa maelekezo kwamba ndani ya mwezi huu ianze. Ni mradi wa uchimbaji wa bwawa la maji uliopo Bumbwini Makoba. Tumesema ndani ya mwezi huu uanze na utaanza kwa ajili ya kunufaisha wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala la piliā€¦

SPIKA: Kwa kifupi.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, Zanzibar inapata ushirikiano mkubwa kushirikishwa kutoka Serikali ya Jamhuri katika vikao vinavyohusina na mazingira katika mambo ya Kimataifa. Hivi karibuni tulikuwa tuna kikao cha COP27 Mkutano wa Kimataifa ambapo Zanzibar tulishiriki. Tanzania tulishiriki lakini Zanzibar walileta delegation yao, tulikuwa na Mkurugenzi wa Mazingira na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha kuonesha kwamba tunao ushirikiano wa karibu baina ya Serikali mbili hizi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. (Makofi)