Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 3 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 42 2023-02-02

Name

Suleiman Haroub Suleiman

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. SULEIMAN HAROUB SULEIMAN aliuliza: -

Je, ni kwa kiasi gani Taasisi za Serikali ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zinashirikiana katika shughuli za kiuchumi?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS,, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira naomba kujibu swali la Mheshimiwa Suleiman Haroub Suleiman, Mbunge kutoka Baraza la Wawakilishi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Taasisi za SMT na SMZ zina ushirikiano wa kuridhisha katika shughuli za kiuchumi ambapo kupitia miradi na program mbalimbali, taasisi zetu za SMT na SMZ zimekuwa zikishirikiana katika shughuli za kiuchumi hasa kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Mzunguko wa Pili, mradi wa kuongeza tija na uzalishaji wa zao la mpunga; mradi wa udhibiti uvuvi na maendeleo shirikishi Kusini Magharibi ya Bahari ya Hindi; mradi wa kuhimili mabadiliko ya tabia nchi kwa kutumia mifumo ikolojia vijijini; Mkakati wa Kudhibiti Sumu Kuvu Tanzania; na Programu ya Maboresho ya Usimamizi wa Fedha.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru (Makofi)