Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwanusuru wananchi wa Manispaa ya Mtwara dhidi ya vumbi la makaa ya mawe?

Supplementary Question 1

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, hii dust suppression system inapunguza vumbi kwa kiasu kidogo sana, lakini pia ukienda bandarini pale utakuta maji yameshakuwa meusi kutokana na hili vumbi. Swali langu la kwanza: Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba inatunza au inalinda vyanzo vya maji ili kusudi visiweze kuathirika kutokana na yale maji ya mvua yanayotiririka ambayo tayari yameshakuwa na vumbi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili: Je, Serikali itakuwa tayari kupokea ushauri kwamba haya makaa ya mawe kutoka kwenye migodi yawe yakisafirishwa yakiwa yamefungwa kwenye vifungashio, kwa mfano, labda viroba au maboksi ili kusudi kuzuia lile vumbi lisitimke wakati wa usafirishaji, wakati wa kushusha mzigo na vile vile wakati wa kupakia mzigo katika meli? Ahsante. (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba swali la Mheshimiwa Anastazia James Wambura, Mbunge wa Viti Maalum, kutoka Mkoa wa Mtwara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Usimamizi na Utunzaji wa Vyanzo vya Maji imewaelekeza watu wote, makampuni, taasisi zote zinazofanya shughuli zote ambazo zitakuwa zinagusia sehemu zenye maji au vyanzo vya maji; tumeshawaelekeza pamoja na hawa wa Mtwara wanaofanya biashara hiyo. Kwanza tumewaelekeza kwa kuwapa taaluma, lengo na madhumuni, watunze vyanzo vya maji. Pia tumekuwa tunasimamia sheria kwa kushirikiana na wenzetu wa NEMC, watu wa Halmashauri na wengine. Lengo na madhumuni ni watu watunze vyanzo vya maji.

Mheshimiwa Spika, pia tumeshakaa nao kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunachukua hatua mbalimbali, na tayari zipo hatua ambazo NEMC wamezichukua kwa baadhi ya watu hawa. Hapa nataka nitoe wito kwa Watanzania wote wanaofanya shughuli za kibinadamu karibu na vyanzo vya maji, wahakikishe kwamba wanatunza vyanzo vya maji. Kinyume na hapo, sheria na taratibu zitakuwa zinachukuliwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala la pili, tupo tayari, tumepokea huo ushauri. Ingawa makaa ya mawe haya yanakuwa ni mawe makubwa, lakini tutajua namna ya kuwashauri wafanyabiashara wawe wanaweka katika package maalum ili yaweze kupunguza hilo vumbi ambalo linaweza kuathiri afya za wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. (Makofi)

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwanusuru wananchi wa Manispaa ya Mtwara dhidi ya vumbi la makaa ya mawe?

Supplementary Question 2

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Suala la makaa ya mawe kutoka Ngaka kupita Songea – Tunduru mpaka Mtwara kuna baadhi ya madereva wamekuwa na tabia ya kusambaza yale makaa ya mawe barabarani, aidha kwa magari kuanguka au kwa kutokufunika. Hii imekuwa ni hatari sana kwa wananchi wanaokaa karibu na barabara hizi. Je, Serikali iatoa kauli gani kwa hawa madereva wanaofanya tabia hii ya kusambaza makaa ya mawe barabarani? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Daimu Mpakate, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hii ni changamoto, tumeiona na mara kadhaa tumekuwa tukikaa na wafanyabiashara hawa pamoja na vyombo vingine au taasisi nyingine zinazohusika ili kuwaeleza hawa wafanyabiashara kwamba wasiyatawanye ama wasiyaweke makaa ya mawe haya katika maeneo tofauti, bali wawe na vituo maalum vya kuweka ili kuepusha athari zinazojitokeza zikiwemo hizo za uchafuzi wa mazingira.

Mheshimiwa Spika, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaendelea kutoa taaluma na kuwaambia wananchi wasiyasambaze haya mwisho wa siku yakawa yanaleta athari. Nakushukuru. (Makofi)

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwanusuru wananchi wa Manispaa ya Mtwara dhidi ya vumbi la makaa ya mawe?

Supplementary Question 3

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Katika Kata ya Wazo, Mkoa wa Dar es Salaam, kuna Kiwanda cha Twiga Cement ambacho kinatiririsha vumbi jingi kuelekea kwa makazi ya wananchi: Nini mkakati wa Serikali kuwanusuru wananchi hawa kuhakikisha hawapati athari za kiafya? Ahsante. (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la moja la nyongeza kutoka kwa Mheshimiwa Felista Njau, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hili jambo tumekuwa tunalipigia kelele sana na hasa hivi viwanda ambavyo vipo karibu na makazi ya wananchi. Tumekuwa tunalisemea sana na tumeshachukua hatua nyingi za kinidhamu lakini pamoja na hayo. tumeshakuwa tunakaa na wamaliki wa viwanda hivi na pia tumekuwa tunawapa taaluma.

Mheshimiwa Spika, nimwambie tu Mheshimiwa kwamba jambo hili tunaendelea kulifanyia kazi ili tuhakikishe kwamba wananchi wanaendelea kuwa salama kutokana na hizi adha na changamoto za viwanda ambazo zinaweza zikawaathiri wananchi kwa njia moja ama nyingine, nakushukuru.