Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 3 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 41 2023-02-02

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwanusuru wananchi wa Manispaa ya Mtwara dhidi ya vumbi la makaa ya mawe?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anastazia James Wambura, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali tayari imeshachukua jitihada za kuweka miundombinu ya kupunguza vumbi la makaa ya mawe ili kuwanusuru wananchi. Tayari Mamlaka ya Bandari Tanzania imefunga mfumo maalum wa dust suppression system unaotumia maji kupunguza vumbi. Pia, limetengwa eneo maalum kwa ajili ya kujenga conveyor belt itakayotumika kupakia makaa ya mawe katika meli. Aidha limetengwa eneo maalum nje ya mji takribani kilometa 34 katika Kijiji cha Kisiwa Mgwao kutoka Mtwara Mjini kwa ajili ya kuhifadhi mizigo ya namna hiyo. Hatua hii itasaidia kupunguza, kusambaa kwa vumbi katika mazingira.

Mheshimiwa Spika, napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kuwa Ofisi ya Makamu wa Rais kupitia NEMC, kwa kushirikiana na Manispaa ya Mtwara na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), kwa pamoja tunaendelea kufuatilia na kusimamia usafirishaji wa uhifadhi wa mazingira katika maeneo hayo, nakushukuru. (Makofi)