Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Soko, Stendi, Dampo na Machinjio na barabara kilomita 12 za lami kupitia TACTIC katika Mji wa Mbulu?

Supplementary Question 1

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, Halmashauri ya Mji wa Mbulu iliko soko na stendi ni mahali pamoja kwenye kiwanja kimoja hali inayohatarisha watumiaji wa huduma na wapokea huduma katika eneo hilo.

Swali la kwanza; je, Serikali haioni kuwa kuna umuhimu mkubwa wa Halmashauri ya Mji wa Mbulu kusogezwa kwenye kundi la pili?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa tatizo hili ni kubwa na tumesubiri mradi huu kwa muda mrefu, Mheshimiwa Waziri ana kauli gani ya kuweza kufika Mbulu na wataalam wa TAMISEMI ili waone tatizo lenyewe kwa undani?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zacharia Paulo Issaay, Mbunge wa Mbulu Mjini , kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kikubwa ni kwamba makundi yote matatu yatapatiwa hizo fedha za TACTIC na miradi yote iliyoainishwa itajengwa. Jukumu kubwa tunalolifanya Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa sasa ni kuhakikisha miradi hii inatekelezeka kama ambavyo imepangwa katika mkakati tulionao. Niwahakikishie tu hata wale wa tier one kwa maana ya kundi la kwanza, miradi yao inaanza kutekelezeka katika mwaka huu wa fedha.

Mheshimiwa Spika, kuhusu miradi kuchelewa, niko tayari kwenda Mbulu pamoja na wataalam kwenda kujionea haya ambayo Mheshimiwa Mbunge anayazungumza, ahsante sana.

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Soko, Stendi, Dampo na Machinjio na barabara kilomita 12 za lami kupitia TACTIC katika Mji wa Mbulu?

Supplementary Question 2

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Je, ni lini Serikali itakamilisha kwa maana ya Mradi huu wa TACTIC kilometa 15 Mji wa Mpanda, Soko la Kazima na kilomita 29 kutoka Mwankulu mpaka Mpanda?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Sebastian Kapufi Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Manispaa ya Mpanda ipo katika kundi la pili ambalo kwa sasa mwezi wa Pili huu tulioanza zabuni za kutafuta wataalam washauri zinaanza na utekelezaji wa miradi hiyo kwa wenzetu watu wa Mpanda utaanza mwakani mwezi Aprili, 2024. (Makofi)

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Soko, Stendi, Dampo na Machinjio na barabara kilomita 12 za lami kupitia TACTIC katika Mji wa Mbulu?

Supplementary Question 3

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mradi wa TACTIC pia upo kwenye Jimbo la Arusha Mjini na mnategemea kujenga stendi ya kisasa Bondeni City na lami maeneo ya Engosheraton na Olasiti na kwa kuwa mradi huu ulitegemea kuanza toka Julai, 2022. Je, ni nini changamoto inayochelewesha mradi huu kuanza kwa wakati maana miezi saba imeshapita mpaka sasa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mrisho Gambo, Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tulichelewa kidogo kwa sababu ya zile taratibu ambazo tulipaswa kuzifuata, lakini mpaka sasa tuko katika hatua nzuri. Kwa mfano, Jiji la Arusha lipo katika kundi la kwanza ambalo mwezi Februari, mwezi huu ambao tuko sasa, Serikali inatangaza kuwapata Wakandarasi watakaoanza kutekeleza na tunatarajia mchakato huu utakamilika mwezi Aprili na wakandarasi watakuwa site kujenga. Kwa hiyo, nimhakikishie Mbunge kwamba utekelezaji katika kundi la kwanza unaanza mwaka huu. (Makofi)

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Soko, Stendi, Dampo na Machinjio na barabara kilomita 12 za lami kupitia TACTIC katika Mji wa Mbulu?

Supplementary Question 4

MHE. JERRY W. SLAA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Barabara ya Banana – Kitunda – Kivule - Msongola inayoenda hospitali ya wilaya kilometa 11.7 ina hali mbaya sana.

Je, Waziri na nimemwona Waziri mwenye dhamana yupo atakuwa tayari baada ya Bunge hili kuambatana na mimi kwenda kutoa majibu ya Serikali, lini barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi na napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jerry Slaa kuhusiana na barabara ya kilometa 11 ya kutoka Banana kwenda Msongola na nimhakikishie kwamba mwezi huu wa Februari tutakapomaliza Bunge atakapokuwa tayari tutaongozana naye kwenda kuangalia barabara hiyo na kuitekeleza, ahsante. (Makofi)