Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 40 2023-02-02

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: -

Je ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Soko, Stendi, Dampo na Machinjio na barabara kilomita 12 za lami kupitia TACTIC katika Mji wa Mbulu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zacharia Paulo Issaay Mbunge wa Jimbo la Mbulu Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Mji wa Mbulu ipo kwenye kundi la tatu lenye miji 18 ambayo utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa stendi kuu ya mabasi, soko jipya na barabara kwa kiwango cha lami unatarajiwa kuanza mwaka huu wa fedha 2022/2023 kwa kuandaa mipango kabambe (master plans).

Mheshimiwa Spika, hivi sasa Ofisi ya Rais, TAMISEMI imeanza kupokea taarifa za hatua mbalimbali za utambuzi wa mipaka ya kila mji pamoja na taarifa nyingine kwa ajili ya kuandaa hadidu za rejea ili kuwapata Washauri waliobobea katika kuandaa mipango kabambe.

Mheshimiwa Spika, baada ya kukamilisha maandalizi ya mipango kabambe, kazi ya usanifu kwa halmashauri za kundi hili utaanza mwaka ujao wa fedha 2023/2024 na kazi za ujenzi zinategemea kuanza katika mwaka wa fedha 2024/2025.