Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: - Je, ni lini mnara wa mawasiliano ya simu utajengwa Kata ya Mamba Kusini Jimbo la Vunjo?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER E. MALLEKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa majibu ya Serikali, lakini nina swali moja la nyongeza. Ni kweli kabisa Kampuni za Vodacom na Tigo zinatoa huduma katika kata hii, lakini kutokana ukuaji wa shughuli za kiuchumi katika kata hii, maeneo mengi yamekuwa na changamoto ya mawasiliano. Je, ni lini sasa Serikali itahakikisha inashughulikia changamoto hiyo ikiwa ni pamoja na kuweza kuwezesha Kampuni ya Airtel na yenyewe inaweka minara katika kata hii? Ahsante.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Edwin Malleko, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa Serikali kupitia utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ni kuhakikisha kwamba inaboresha mazingira ya mawasiliano nchini kote. Vile vile kwa kuangalia katika jibu langu la msingi hasa hasa katika Kata hii ya Mamba tayari kuna mnara mwingine ambao unajengwa katika kata hii ambapo naamini kabisa utakapokamilika suala la mawasiliano litakuwa limeboreka kabisa, ahsante.

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: - Je, ni lini mnara wa mawasiliano ya simu utajengwa Kata ya Mamba Kusini Jimbo la Vunjo?

Supplementary Question 2

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru. Naipongeza Serikali na hasa katika Jimbo langu la Nkenge wilaya ya Misenyi. Ndani ya kipindi cha mwaka mmoja nimejengewa minara minne na hivyo kupunguza tatizo la mawasiliano. Hata hivyo, kama tunavyojua Jimbo la Nkenge linapakana na nchi ya Uganda muda mwingi tunapata mawasiliano ya simu na redio kutoka nchi Jirani. Je, ni lini sasa Serikali itaendelea kumaliza changamoto ya minara katika kata nyingine zilizobaki? Ahsante.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa sababu nakumbuka tulifanya ziara mpakani kule, tukatembea wote, tukajionea hali halisi. Baada ya kuona hiyo hali ya changamoto ya mawasiliano, Serikali iliamua kumpelekea minara minne ambayo Mheshimiwa Mbunge ameitaja. Kwa hiyo tumpongeze Mheshimiwa Rais kwa kuridhia kuleta fedha kwa ajili ya ujenzi wa minara katika Jimbo la Misenyi. Ahsante.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: - Je, ni lini mnara wa mawasiliano ya simu utajengwa Kata ya Mamba Kusini Jimbo la Vunjo?

Supplementary Question 3

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona. Katika Jimbo la Kilwa Kaskazini Serikali imefanya kazi kubwa ya kujenga minara 37 katika vijiji 37 vya Jimbo letu la Kilwa Kaskazini na hivyo vijiji 16 vimebaki vikiwa havina mawasiliano ya simu za mkononi.

Je, ni lini Serikali itajenga mitandao ya mawasiliano ya simu ya mkononi katika vijiji hivyo 16 vilivyobaki?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Kilwa Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, upatikanaji wa huduma ya mawasiliano katika jimbo hili ni zaidi ya asilimia 70 na sasa Wizara yetu kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote imeandaa timu ya kuzunguka nchi nzima na kufanya tathimini na kuangalia maeneo yote ambayo bado yana changamoto ya mawasiliano ili yaweze kuingizwa kwenye utaratibu wa utekelezaji. Kwa hiyo, naamini kabisa timu hii itakapokamilisha kazi yake, basi tunaamini kwamba bajeti tutakayoileta hapa itakuwa inatazama kwa mapana kulingana na matatizo ya changamoto ambazo zitakuwa zimetokea katika Jimbo la Kilwa Kaskazini. Ahsante.