Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 2 Works, Transport and Communication Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 30 2023-02-01

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: -

Je, ni lini mnara wa mawasiliano ya simu utajengwa Kata ya Mamba Kusini Jimbo la Vunjo?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Esther Edwin Malleko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kata ya Mamba Kusini inaundwa na Vijiji vya Mkolowony, Lekura, Kiria, Kimbogho na Kimangara. Katika jitihada za Serikali za kufikisha huduma za mawasiliano katika maeneo mbalimbali nchini kwa kushirikiana na watoa huduma, Kampuni za Tigo na Vodacom zinatoa huduma za mawasiliano katika kata hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, Serikali itafanya tathimini katika Kata hii ya Mamba ili kubaini changamoto zilizopo za mawasiliano ya simu na kuchukua hatua stahiki ikiwemo kuyaingiza maeneo ya kata hii yatakayobainika kuwa na changamoto ya upatikanaji wa huduma za mawasiliano ya uhakika katika orodha ya vijiji vitakavyoingizwa katika zabuni zijazo. Ahsante.