Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Anania Tadayo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Primary Question

MHE. JOSEPH A. TADAYO aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kuweka sharti vikundi vya wanawake na vijana kuwa na mtu mwenye ulemavu kwa mikopo ya Halmashauri?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH A. TADAYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina swali moja la nyongeza.

Kwa kuwa baadhi ya watu wenye ulemavu wanapata changamoto ya kufanya biashara wakiwa peke yao pengine kutokana na nature na ile hali ya ulemavu wao na kwa kuwa imejidhihirisha kwamba Halmashauri nyingi zinakosa wakopaji wa kutosha katika kundi hili la walemavu na hivyo kupelekea zile fedha kukopeshwa kwenye makundi mengine au hata kurudishwa. (Makofi)

Je, Serikali ina mpango gani basi wa kuwarahisishia zaidi hawa watu wenye ulemavu ili waweze kutumia ile asilimia mbili yao ambayo wamewekewa kwa mujibu wa sheria? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Joseph Anania Tadayo, Mbunge wa Jimbo la Mwanga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kasi ya ukopaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa kundi la watu wenye ulemavu bado hairidhishi na Serikali tumeona hilo na moja ya sababu ni kwamba walio wengi hawana ile confidence ya kukopa wakiamini kwamba hawawezi kurejesha. Lakini ni hatua ambazo Serikali imechukua kwanza ni kuendelea kutoa elimu na hamasa kwa watu wenye ulemavu; lakini pili kuwarahisishia kwamba hata mtu mmoja mwenye ulemavu anaweza akapata mkopo wa asilimia 10 akafanya biashara yake baada ya Kamati ya Mikopo kujiridhisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nitumie fursa hii kuhamasisha wananchi, lakini kuwaelekeza watendaji kuendelea kuhamasisha na kutoa elimu kwa makundi ya watu wenye ulemavu ili wapate mikopo ya asilimia 10, ahsante.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH A. TADAYO aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kuweka sharti vikundi vya wanawake na vijana kuwa na mtu mwenye ulemavu kwa mikopo ya Halmashauri?

Supplementary Question 2

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa shida kubwa sana inayopata watu wenye ulemavu hasa wenye uoni hafifu, Serikali haioni umuhimu sasa wa kutengeneza document zenye nukta nundu ili hawa watu wanaopata shida ya kusoma waweze kujua taarifa za mikopo katika Halmashauri zetu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sophia Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja hii ni muhimu na sisi tunaichukua kwa ajili ya kuifanyia kazi ili kukwawezesha watu wenye ulemavu au uoni hafifu waweze kupata uwezo wa ku-access taarifa hizo kupitia taarifa za nukta nundu, ahsante sana.