Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 24 2023-02-01

Name

Joseph Anania Tadayo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Primary Question

MHE. JOSEPH A. TADAYO aliuliza: -

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuweka sharti vikundi vya wanawake na vijana kuwa na mtu mwenye ulemavu kwa mikopo ya Halmashauri?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Anania Tadayo, Mbunge wa Jimbo la Mwanga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mikopo inayotokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri hutolewa kwa mujibu wa Sheria za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu ya mwaka 2019 na Kanuni zake zilizoboreshwa mwaka 2021.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa masharti yaliyowekwa kwenye kanuni hizo, hazizuii mtu mwenye ulemavu kuwa miongoni mwa vikundi vya wanawake au vijana ikiwa amekidhi mahitaji ya sheria na kanuni zake. Aidha, kundi la watu wenye ulemavu limepewa fursa mahususi ili kuwarahisishia kupata mikopo ya asilimia 10, ahsante.