Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga soko la Tengeru kwa kiwango cha Kimataifa?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Mwenyekiti nashukuru, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, lakini mazingira pale kwenye lile soko na fedha zinazobadilishwa wakati wa biashara pale ambazo ni nyingi sana zinahitaji kuweka miundombinu ikae vizuri kidogo.

Je, Serikali iko tayari kwenda kujenga shade kama machinga complex ya Dodoma pale kwa ajili ya kunusuru akina mama ambao wanachomwa na jua wakati wa jua kali?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Halmashauri ilitumia takribani Milioni 11 kwa ajili ya kuweka stendi ndogo pale ambayo inaweza ikaingiza mabasi 12. Je, Serikali haioni kwamba ni muhimu sasa kuingilia kati na kujenga ile barabara ya kutokea kwa sababu kibali cha kutumia ile stendi bado hakijatoka kutokana na barabra kutokukidhi viwango. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. John Danielson Pallangyo, Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kufatilia suala la soko lile la Tengeru, lakini utaratibu wa Serikkali ni kwamba tumetafuta eneo jingine kubwa zaidi haina maana kwamba tunaliacha kabisa lile eneo ambalo tayari kwa sasa linatumika kama gulio. Kwa hiyo, ninatoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri hii ili watenge fedha kwenye mapato ya ndani kuboresha soko hilo, kwa maana kuweka miundombinu rafiki kwa wafanyabiashara, pia kupitia TARURA Halmashauri hii watenge fedha kwa ajili ya kuboresha barabara hiyo ambayo itawezesha kujenga uwezo wa wananchi kufanya biashara kwa ufanisi mkubwa zaidi. Ahsante. (Makofi)