Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 25 2023-02-01

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga soko la Tengeru kwa kiwango cha Kimataifa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. John Danielson Pallangyo Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa kuwa na soko la kisasa kutokana na ongezeko kubwa la shughuli za kiuchumi katika eneo la Tengeru. Kwa sasa eneo hilo lenye ukubwa wa ekari 2.3 linatumika kama gulio.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na uhitaji uliopo eneo hilo ni dogo na halikidhi mahitaji ya soko hilo. Hivyo, Halmashauri ya Meru imetenga eneo la Madiira lenye ukubwa wa ekari 15.5 lenye uwezo wa kubeba miundombinu yote ikiwemo miundombinu kwa ajili ya wafanyabiashara wadogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri inatarajia kukamilisha na kuwasilisha andiko la mradi huo wa kimkakati Ofisi ya Rais, TAMISEMI Februari, 2023 kwa ajili ya maombi ya fedha, ahsante.