Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA K.n.y. MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya kutoka Kata ya Katoma kwenda Nyambaya utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Ikumbukwe kwamba Halmashauri hizi za Geita ni miongoni mwa Halmashauri ambazo zinachangia mapatao makubwa sana Serikalini kutokana na masuala ya uchimbaji wa dhahabu. Kwa hiyo, barabara hizi zinapokuwa hazitengenezwi vizuri hazitoi taswira nzuri kwa wananchi wa maeneo hayo. Kwa hiyo, naomba kuisisitiza Serikali kuongeza jitihada katika kuikamilisha vizuri barabara hii.

Mheshimiwa mwenyekiti, swali la pili ni kwamba, inaonekana katika Halmashauri nyingi amabazo ziko Vijijini na zile ambazo zinaanza kuchipukia zisizo na mapato makubwa, ugawaji wa fedha inayopelekwa kwa ajili ya barabara hizi za TARURA ni mdogo sana kiasi kwamba barabara nyingi zinashindwa kufunguliwa.

Je, ni lini Serikali itaeweka utaratibu mzuri wa kuongeza jitihada za kufungua maeneo haya ya vijijini ili wananchi waweze kupata huduma inayostahili? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili madogo ya nyongeza ya Mheshimiwa Stella Manyanya, Mbunge wa Jimbo la Nyasa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa Halmashauri ya Geita kutokana na shughuli za kiuchumi ambazo ziko pale na ndiyo maana ukiangalia kwenye jibu letu la msingi tumetenga fedha na tutakacho hakikisha ni kwamba fedha hizo zinakwenda na zile barabra zinarekebishika, kwa hiyo hilo halina shaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili kuhusu ugawaji wa fedha za barabara ambazo zimekuwa zikionekana kuwa chache na kwa sababu ya ukubwa wa mtandao wa barabara tulionao nchini Serikali tunalipokea ombi la Mheshimiwa Mbunge na tutalizingatia kulingana na bajeti ambavyo tutakuwa tukizitenga, ahsante. (Makofi)