Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 21 2023-02-01

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA K.n.y. MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi wa barabara ya kutoka Kata ya Katoma kwenda Nyambaya utaanza?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Kasheku Musukuma, Mbunge wa Jimbo la Geita, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Katoma kwenda Nyambaya ina urefu wa kilomita 6.3 ambapo katika mwaka wa fedha 2021/2022 ilianza utekelezaji wa ujenzi wa barabara hii kwa kujenga makalavati manne kwa gharama ya shilingi milioni 22.40 kwa fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Aidha, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali itatenga bajeti ya Shilingi Milioni 67.2 kuendelea na ujenzi wa barabara hiyo kupitia fedha za Mfuko wa Barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga fedha katika bajeti zake za kila mwaka kwa ajili ya matengenezo na ujenzi wa barabara za Wilaya ya Geita ikiwemo barabara ya Katoma hadi Nyambaya kulingana na upatikanaji wa fedha.