Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: - Je, Serikali haioni kuna haja ya nchi yetu kurudi COMESA?

Supplementary Question 1

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, ikiwa Jumuiya hizi zinapoanzishwa kila Jumuiya inakuwa na lengo lake. Mfano, SADC ukisoma malengo yake ilianzishwa kwa ajili ya siasa na usalama zaidi wa nchi zetu. Ikiwa kama COMESA ilianzishwa kwa ajili ya kuwepo kwa soko la pamoja na katika majibu ya msingi kwenye swali inasema kwamba kuwepo kwa tripartite arrangement kunachangia kuondoa changamoto hizi.

Je, mbona bado wafanyabiashara wetu wanapotaka kuyaendea masoko ya hizo nchi ambao ni wanachama na ambao sisi siyo wanachama, wanaendelea kupitia changamoto. Mfano, wafanyabiashara wa Tanzania wanapotaka kuliendea soko la Congo wanakutana na changamoto nyingi lakini hata mazao yanapokuwa yanauzwa kwenye nchi mfano Misri, tunapata tozo kubwa ya ushuru wa bidhaa zaidi ya 30%.

Swali la pili, je, Serikali haioni sasa ipo haja kwa umuhimu kabisa kwamba toka tujitoe kwenye COMESA mwaka 2000 na sasa hivi ni miaka 13, Serikali inaonaje iende kufanya utafiti kukaa na wafanyabiashara ambao wanafanya biashara kwenye nchi hizi wanachama, zituletee zipi faida ambazo sisi tulipata kutoka kwenye COMESA na zipi hasara ambazo nchi imepata katika kipindi cha miaka 13 kujitoa kwenye COMESA? (Makofi)

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Condester Michael Sichalwe, Mbunge wa Momba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza ninampongeza Mheshimiwa Mbunge kwani amekuwa mfuatiliaji mkubwa sana katika masuala ya biashara hasa baina ya sehemu anakotoka huko Momba na soko la DRC. Nianze kwanza na swali la pili alilosema kuhusu utafiti, tuangalie utafiti au tufanye utafiti na tuone kama tumeathirika au hatujaathirika na Tanzania kujitoa katika COMESA.

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kabla ya Tanzania kujitoa COMESA, ilifanya utafiti mkubwa sana na kujiridhisha kwamba hakuna hasara yoyote na hakuna athari yoyote ya Tanzania kujitoa COMESA.

Mheshimiwa Spika, swali la pili kuhusiana na changamoto ambazo zipo hasa katika soko la Congo. Changamoto hizi hazitokani kabisa na Tanzania kujitoa COMESA. Changamoto na vikwazo vya kibiashara ambavyo siyo vya kiforodha zimekuwepo katika nchi mbalimbali na kila zinapojitokeza basi hushughulikiwa kwa kadri inavyowezekana.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana specific na suala la Congo -DRC ni kwamba, Tanzania imechukua hatua nyingi sana za kuhakikisha kwamba wafanyabiashara wetu hawapati vikwazo wanapofanya biashara nchini Congo. Hatua hizo ni kwanza kuhakikisha JPC ambayo ni uhusiano wa kibiashara kati ya DRC na Tanzania na ni mwezi Septemba tu last year JPC ilikutana na ilizungumzia masuala mbalimbali ya kukuza biashara. Ahsante sana. (Makofi)