Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 1 Foreign Affairs and International Cooperation Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki 16 2023-01-31

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: -

Je, Serikali haioni kuna haja ya nchi yetu kurudi COMESA?

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano na Afrika Mashariki, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Condester Michael Sichalwe, Mbunge wa Momba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Tanzania ilikuwa miongoni mwa nchi 19 zilizokuwa mwanzilishi wa Jumuiya ya Soko la Pamoja la Mashariki na Kusini mwa Afrika (COMESA) mwaka 1994. Tanzania ilijitoa katika COMESA mwaka 2000 kwa sababu ilikuwa ni mwanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), ambapo baadhi ya nchi za jumuiya hizo pia ni wanachama wa COMESA.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kujitoa kwa Tanzania kulifikiwa baada ya kujiridhisha kuwa nchi haitaathirika kiuchumi, kwani bado ni mwanachama wa EAC na SADC na kuwa lengo ni kulipunguzia Taifa gharama hasa michango ya wanachama.

Mheshimiwa Spika, tutakumbuka kuwa, mwaka 2008 nchi za COMESA, EAC na SADC zilikubaliana kuanzisha Utatu. Hivyo Tanzania inaendelea kushirikiana na COMESA kupitia Utatu huu (COMESA – EAC - SADC Tripartate Arrangement). Aidha, mwezi Septemba, 2021, Bunge lako Tukufu liliridhia Mkataba wa kuanzisha Eneo Huru la Biashara la Bara la Afrika (AfCFTA). Kuwa sehemu ya Utatu wa COMESA – EAC - SADC, na kuridhiwa kwa Mkataba wa AfCFTA kunaifanya Tanzania kuendelea kushirikiana na nchi za COMESA. Ahsante sana.