Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, hadi sasa mpango wa kutatua kero ya maji katika Mji wa Tunduma umefikia hatua gani?

Supplementary Question 1

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Spika, kwanza nishukuru sana kwa majibu ya Serikali; lakini naomba nitoe ombi moja, kwamba niombe waharikishe sana kuweza kupatikana kwa huyo mkandarasi ili kuweza kuwapunguzia adha ya maji wanawake wenzangu wa Mji wa Tunduma, Mji wa Vwawa pamoja na Mji wa Mlowo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitakuwa na swali moja la nyongeza. Hali ya upatikanaji maji katika Wilaya ya Songwe ambayo ina kata 18 ikiwepo Kata ya Mkwajuni, Kata ya Saza pamoja na Galula sio ya kuridhisha, naomba nipate kauli ya Serikali kwamba ina mpango gani wa kuboresha hali ya upatikanaji maji katika Wilaya ya Songwe, ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Juliana Shonza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote, nipende kupokea pongezi zake, nawe nakupongeza kwa kuwa mfuatiliaji mzuri wa masuala ya maji ili kuhakikisha mwanamke anatuliwa ndoo kichwani.

Mheshimiwa Spika, kuharakisha kupata mkandarasi, hii ni moja ya jitihada tunayoifanya Wizara. Nikuombe Mheshimiwa Mbunge tuendelee kushirikiana kuhakikisha tunakwenda sambamba na lengo la kumtoa mama ndoo kichwani linakamilika kwa wakati. Maeneo ya Wilaya ya Songwe, Mkwajuni na Kisasa, tayari Serikali inaendelea na jitihada mbali mbali kuhakikisha matatizo ya maji katika maeneo haya tunakwenda kuyafanyia kazi.

Mheshimiwa Spika, miezi michache iliyopita gari la uchimbaji visima lilikuwa kule Wilayani Songwe na liliweza kufanya kazi ya uchimbaji visima katika maeneo kadhaa. Kazi hii itaendelea, lengo ni kuona visima vile tunavipata, tupate vyanzo vya maji ili tuweze kusambaza maeneo yote ambayo bado yanaathirika na tatizo la maji. (Makofi)